Imran Khan aapishwa kama waziri mkuu mpya wa Pakistan
https://parstoday.ir/sw/news/world-i47519-imran_khan_aapishwa_kama_waziri_mkuu_mpya_wa_pakistan
Nyota wa zamani wa mchezo wa cricket nchini Pakistan amechukua nafasi ya waziri mkuu mpya wa nchi hiyo kufuatia idhini ya bunge.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Aug 18, 2018 02:52 UTC
  • Imran Khan aapishwa kama waziri mkuu mpya wa Pakistan

Nyota wa zamani wa mchezo wa cricket nchini Pakistan amechukua nafasi ya waziri mkuu mpya wa nchi hiyo kufuatia idhini ya bunge.

Khan, mwenye umri wa miaka 65, ameapishwa leo kama Waziri Mkuu wa 22 wa Pakistan katika sherehe iliyohudhuriwa na viongozi kadhaa na wachezaji wa cricket mjini Islamabad.

Chama cha Khan cha Pakistan Tehreek-e-Insaf (PTI) kilishinda uchaguzi wa bunge uliofanyika Julai lakini hakikuweza kupata ushindi mutlaki wa kuunda serikali na kwa msingi huo  inatazamiwa kuwa ataunda serikali ya mseto.

Katika ucahguzi uliofanyika bungeni jana, Khan alipata kura 176 huku mpinzani wake wa karibu Shehbaz Sharif wa chama cha Pakistan Muslim League-Nawaz (PML-N) akipata kura 96 tu.

Imran Khan baada ya kupiga kura

Wapinzani wanadai kuwa uchaguzi wa bunge wa Julai 25 ulikumbwa na wizi wa kura uliotekelezwa na jeshi la nchi hiyo ambalo limewahi kutawala nchi hiyo kwa miongo kadhaa. Hata hivyo jeshi limepinga tuhuma hizo.