-
Utafiti: UK inaendelea kusakamwa na uchochole
Jan 29, 2026 02:35Umaskini nchini Uingereza umezidi kuwa mbaya, huku idadi kubwa ya watu wakiishi katika hali ngumu wasiweze kumudu mahitaji yao ya msingi, hayo ni kwa mujibu utafiti uliofanywa na shirika moja la kutoa misaada.
-
Mdororo wa uchumi US; UPS kuwafuta kazi watu 30,000
Jan 28, 2026 23:54Kampuni ya kusafirisha mizigo ya United Parcel Service (UPS) ya Marekani imetangaza kwamba, itawatimua kazi watu 30,000 zaidi mwaka huu, katika juhudi za kupunguza ushirikiano wake na shirika la Amazon, ikiwa ni sehemu ya kutekeleza mpango wake wa 'uokoaji' na kubana matumizi.
-
Rais wa Ukraine aliagiza jeshi liue 'makumi ya maelfu ya Warusi'
Jan 28, 2026 06:49Jeshi la Ukraine linapaswa lijikite katika kusababisha vifo vingi zaidi kwa Russia kadiri iwezekanavyo. Hayo yametamkwa na Rais wa Ukraine Vladimir Zelensky na kusisitiza kwamba, idadi ya vifo 50,000 vya Warusi kwa mwezi ni "kiwango bora" ambacho wanajeshi wa Ukraine wanapaswa wajitahidi kukifikia.
-
The Guardian: Hofu inayotanda Minneapolis inafanana na ya vita vya wenyewe kwa wenyewe
Jan 28, 2026 00:59Makala ya uchambuzi iliyochapishwa na gazeti la Uingereza la The Guardian imefafanua ilichokielezea kuwa ni eneo la kutisha huko Minneapolis, Minnesota, nchini Marekani na kusema kwamba ni wakati muhimu unaofichua sura ya ufashisti wa wazi chini ya utawala wa Rais Donald Trump.
-
Obama na Clinton wawahimiza Wamarekani 'kusimama' huku maandamano yakiendelea nchini Marekani
Jan 27, 2026 07:26Marais wa zamani wa Marekani, Barack Obama na Bill Clinton, wamewahimiza Wamarekani kusimama na kutetea kile walichokiita "maadili ya msingi ya Marekani" baada mawakala wa uhamiaji wa Shirikisho huko Minneapolis kumpiga risasi na kumuua muuguzi wa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), Alex Pretti.
-
Rais wa zamani wa FIFA: Msiende Marekani kutazama Kombe la Dunia kutokana na wasiwasi wa kiusalama
Jan 27, 2026 06:56Rais wa zamani wa Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA) amewataka watazamaji wa Kombe la Dunia wasisafiri kwenda Marekani kutokana na wasiwasi wa kiusalama.
-
Katibu Mkuu wa UN: 'Sheria ya Msituni' inachukua nafasi ya utawala wa sheria kimataifa
Jan 27, 2026 03:09Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameonya kwamba nidhamu ya dunia inazidi kumomonyoka huku utawala wa sheria ukifutwa, na nafasi yake kuchukuliwa na kile alichokiita "sheria ya msituni."
-
Katibu Mkuu wa NATO: Ulaya 'iendelee kuota' kama inadhani inaweza kujilinda bila ya US
Jan 27, 2026 03:08Katibu Mkuu wa NATO, Mark Rutte amesema, Umoja wa Ulaya, EU bali hata Ulaya nzima haina uwezo wa kujilinda bila ya Marekani na kusisitiza kuwa, nchi wanachama zitalazimika kutumia hadi 10% ya Pato lao la Taifa kwa ajili ya shirika hilo la kijeshi, ambayo inaweza pia isitoshe.
-
Russia yaionya Marekani kuhusu chokochoko yoyote dhidi ya Iran
Jan 26, 2026 23:05Serikali ya Russia imeionya Marekani kuhusiana na kuanzisha chokochoko yoyote ya kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Waandamanaji wakusanyika Marekani baada ya afisa wa uhamiaji kutekeleza mauaji
Jan 26, 2026 23:03Umati wa watu umekusanyika Minneapolis, Marekani kupinga uwepo wa maafisa wa uhamiaji wa shirikisho katika jimbo hilo, baada ya kupigwa risasi na kuuawa Alex Pretti mwenye umri wa miaka 37.