16
Akhlaqi Katika Uislamu (16)
Amani ya Allah, rehma na baraka zake ziwe juu yako mpendwa msikilizaji popote pale ulipo wakati huu. Nakukaribisha kusikiliza sehemu hii ya 16 ya kipindi cha Akhlaqi Katika Uislamu nikiwa na matumaini kuwa, mimi pamoja na wewe tutanufaika na yale tutakayoyasikia katika kipindi hiki. Endelea kuwa nami basi hadi tamati ya mazungumzo yetu, ambayo kwa leo yatahusu umuhimu wa kutimiza ahadi na kujiepusha na mwenendo wa kuvunja ahadi na mapatano.