-
Mamilioni ya watu washiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds kote duniani
Jul 01, 2016 03:23Mamilioni ya watu hapa Iran na katika nchi zingine kote duniani wanashiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds, kuonyesha uungaji mkono wao kwa wananchi madhulumu wa Palestina sambamba na kulaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika ardhi zao unazozikalia kwa mabavu.
-
IRGC:Uchu wa kuikomboa Quds, chachu ya harakati za muqawama
Jun 30, 2016 23:10Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC limesema uchu wa kutaka kukombolewa Quds tukufu ndio chachu inayozipa nguvu harakati za kimuqawama katika eneo hili la Mashariki ya Kati.
-
Wito wa Iran kuelekea Siku ya Kimataifa ya Quds
Jun 30, 2016 03:01Sambamba na kukaribia Siku ya Kimataifa ya Quds itakayoadhimishwa kote duniani kesho Ijumaa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekosoa vikali jinai za kutisha zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran ifuatilie haki zake zilizokiukwa na Marekani
Jun 29, 2016 23:09Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amevitaka vyombo vya mahakama Iran kuchukua hatua imara zaidi katika kufuatilia haki za Iran zilizokiukwa kutokana na vikwazo kupitia vyombo vya mahakama vya kimataifa.
-
MAKALA: Siku ya Kimataifa ya Quds
Jun 29, 2016 04:05Hamjambo wasikilizaji wapenzi na karibuni kuwa nasi katika makala hii maalumu inayokujieni kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Quds. Ni matarajio yangu kuwa mtaendelea kuwa nasi hadi mwisho wa kipindi hiki.
-
Siku ya Kimataifa ya Quds: Palestina, Kadhia Kuu ya Waislamu Duniani
Jun 28, 2016 23:57Mbunge wa ngazi za juu nchini Iran amesema kadhia ya Palestina ndio muhimu zaidi kwa Waislamu na hivyo ametoa wito wa ushiriki mkubwa katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds.
-
Jeshi la Iran launga mkono Intifadha ya Palestina
Jun 28, 2016 09:35Kamandi ya Majeshi yote ya Iran imetoa wito kwa watu wote katika ulimwengu wa Kiislamu kujitokeza kwa wingi katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds Ijumaa hii.
-
Familia: Israel inazuia miili ya Wapalestina wanaowaua
Jun 23, 2016 03:33Familia za Wapalestina waliouawa shahidi na askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamefanya maandamano kuutaka utawala wa Tel Aviv kuwapa miili ya wapendwa wao huku wakitaja sera hiyo ya kuzuia miili kuwa 'jinai na mateso kwa walio hai na waliokufa'.
-
Kamanda mwandamizi Iran aionya vikali Bahrain kwa kumvua uraia Ayatullah Isa Qassim
Jun 21, 2016 03:02Kufuatia hatua ya utawala wa Bahrain kumvua uraia mwanazuoni mashuhuri wa Kiislamu Sheikh Isa Qassim, kamanda wa Kikosi cha Quds katika Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ameuonya vikali utawala wa Aal Khalifa
-
Al Zawawi asisitiza kuendelezwa Intifadha ya wananchi wa Palestina
Jun 16, 2016 02:53Balozi wa Palestina nchini Iran amesema kuwa Intifadha ya wananchi wa Palestina itaendelea hadi kukombolewa Quds Tukufu.