Rais Jacob Zuma: Afrika Kusini imeazimia kufikia ustawi wa kudumu
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i15796-rais_jacob_zuma_afrika_kusini_imeazimia_kufikia_ustawi_wa_kudumu
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amesema kuwa, nchi yake imeazimia kufikia malengo ya ustawi wa kudumu.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Sep 21, 2016 10:42 UTC
  • Rais Jacob Zuma: Afrika Kusini imeazimia kufikia ustawi wa kudumu

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amesema kuwa, nchi yake imeazimia kufikia malengo ya ustawi wa kudumu.

Rais Zuma amesema hayo katika hotuba yake kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani na kusisitiza kwamba, nchi yake imeandaa mipango madhubuti ya kupambana na umasikini, ukosefu wa ajira na kutokuweko usawa wa kijamii.

Rais Zuma amesema kuwa, katika kipindi cha muongo mmoja uliopitya, Afrika Kusini imepiga hatua kubwa katika njia ya kutokomeza mambo ambayo ni sumu ya kufikia ustawi na maendeleo.

Rais Zuma katika moja ya mikutano ya chama tawala cha ANC

Rais wa Afrika Kusini ameashiria mwenendo wa kuzifanya nchi kuwa za viwanda kwamba, ni mkakati katika njia ya ustawi wa Afrika, kupambana na umasikini katika bara hilo na kuongeza kuwa, kuzifanya nchi kuwa za viwanda ni hatua ambayo inaweza kusambaratisha umasikini, ukosefu wa ajira na hata ukosefu wa usawa wa kijamii na hivyo kufungua njia ya ustawi na maendeleo.

Licha ya Afrika Kusini kutajwa kuwa imechukua hatua muhimu za kimaendeleo katika miaka ya hivi karibuni, lakini imekuwa ikikabiliwa pia na ukosefu wa ajira pamoja na kutawaliwa na ufisadi mkubwa serikalii, jambo ambalo limeifanya serikali ya Rais Jacob Zuma kukabiliwa na ukosoaji mkubwa na hata kupungua uungaji mkono wa wananchi kwa chama tawala cha nchi hiyo  ANC.