Zuma: Afrika Kusini inaondokana na mdodoro wa uchumi
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amesema kuwa nchi hiyo hivi sasa inaondoka katika hali ya mdodoro wa kiuchumi.
Rais Zuma ambaye jana alikuwa akihutubia bunge ameeleza kuwa uchumi wa Afrika Kusinihivi karibuni unatarajiwa kuondokana na hali ya kudorora; hali ambayo iliathiri sekta hiyo tangu mwezi Juni mwaka huu. Tangu miaka minane iliyopita hadi hivi sasa, hii ni mara ya kwanza uchumi wa Afrika Kusini unakumbwa na hali ya mdodoro. Rais Zuma amekiri kwamba hali hiyo imeitia wasiwasi mkubwa serikali yake.
Hii ni mara ya kwanza uchumi wa Afrika Kusini unaathiriwa na hali ya mporomoko tangu mwaka 2009 hadi sasa. Katika mwaka huo uchumi wa Afrika kusini ulishuka kufuatia kuwepo pia mgogoro wa fedha kimataifa. Hata hivyo Rais wa Afrika Kusini sasa anasema kuwa anatumai kwamba nchi yake itaondokana na hali hiyo haraka iwezekanavyo.
Chama cha Congresi ya Taifa (ANC ) ambacho ni chama tawala nchini Afrika Kusini kilichukua madarakani tangu mwaka 1994 yaani kuanzia mwaka ule ambapo mfumo wa ubaguzi wa rangi nchini humo (Apartheid) ulihitimishwa rasmi, hata hivyo kwa kuzingatia kufeli kwa sekta ya uchumi ya nchi hiyo, chama hicho kimepoteza pakubwa uungaji mkono wa wananchi.