Vikao vya Bunge la Afrika vyaanza mjini Kigali Rwanda + Sauti
Oct 22, 2018 17:02 UTC
Bunge la Afrika limefungua kikao chake cha wiki mbili mjini Kigali Rwanda ambapo kwa muda wa wiki mbili wabunge wake watajadili mambo kadhaa kuhusu demokrasia,uongozi bora na kurahisisha mafungamano ya biashara baina ya waafrika wenyewe. Ni kikao kilichofunguliwa na Rais Paul Kagame wa Rwanda ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Afrika.
Tags