-
Sisitizo la Amir-Abdollahian la kutatuliwa matatizo kati ya Iran na Afghanistan
Dec 26, 2023 23:22Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya ulazima wa kutatuliwa masuala yaliyopo kati ya Iran na Afghanistan yakiwemo masuala ya mipaka na maji.
-
Radiamali mbalimbali za kuuawa shahidi mshauri wa kijeshi wa Iran nchini Syria
Dec 26, 2023 05:28Kamanda Sayyid Razi Mousavi, mmoja wa washauri wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (SEPAH), ambaye alikuwa akifanya kazi katika uga wa utoaji misaada ya kilojistiki kwa Mhimili wa Muqawama wa Syria, aliuawa shahidi katika shambulio lililofanywa jana Jumatatu na utawala wa Kizayuni katika eneo la Zainabiyah mjini Damascus.
-
Ujumbe wa kuendelea maandamano ya wananchi wa Uturuki dhidi ya Israel
Dec 26, 2023 04:02Licha za siasa za kundumakuwili za serikali ya Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki kuhusu masuala ya Palestina, wananchi wa nchi hiyo bado wanaendelea na maandamano yao ya kihamasa dhidi ya Israeli.
-
Radiamali ya Amir Abdollahian kwa madai ya Marekani kuhusu hatua ya Yemen dhidi ya meli za Israel
Dec 25, 2023 23:09Hossein Amir Abdollahian, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kusisitiza kuwa Iran haina askari wa niaba katika eneo la Asia Magharibi amesisitiza kuwa, Iran haihusiki na mashambulizi ya Yemen dhidi ya meli za Israel.
-
Changamoto zinazoikabili Israel na Marekani za kuendeleza vita vya Gaza
Dec 25, 2023 07:03Katika siku ya 80 ya uvamizi ulioanzishwa na utawala haramu wa Kizayuni dhidi ya Gaza, maafa makubwa linayopata jeshi la utawala huo dhalimu katika vita vya ardhini pamoja na mashambulio makali na makubwa linayofanya jeshi hilo katika maeneo mbalimbali ya Gaza, ni matukio ambayo yangali yanaendelea kushuhudiwa katika eneo hilo.
-
Kuvunjika muungano wa baharini wa Marekani kwa kujiondoa Ufaransa, Uhispania na Italia
Dec 25, 2023 02:22Marekani imetangaza kuunda Muungano wa Baharini ikiwa ni katika jitihada zake za kuendelea kuutetea kwa hali na mali utawala ghasibu wa Israel katika hujuma yake ya kinyama dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza na kukabiliana na mashambulizi ya Yemen katika Bahari Nyekundu dhidi ya meli zinazoelekea katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na Israel huko Palestina.
-
Kufikia kikomo uwepo wa kijeshi wa Ufaransa nchini Niger; ushindi kwa Waniger
Dec 24, 2023 07:40Miezi kadhaa baada ya kutokea mabadiliko ya kisiasa nchini Niger na sisitizo la Baraza la Kijeshi la kuondoka vikosi vya kijeshi vya Ufaransa katika ardhi ya nchi hiyo, hatimaye kundi la mwisho la askari wa Paris liliondoka Niger siku chache zilizopita.
-
Mazungumzo ya kwanza ya simu baina ya Marais wa Iran na Misri; hatua ya kukuza uhusiano
Dec 24, 2023 04:44Jana Jumamosi, Sayyid Ebrahim Raisi, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran alizungumza kwa simu na Rais Abdel Fattah El Sisi wa Misri, ikiwa ni mara ya kwanza kwa marais wa nchi hizi mbili kuzungumza kwa simu na ikiwa ni katika sehemu ya juhudi za kufufua uhusiano wa pande mbili.
-
Jibu na indhari ya Iran kwa msimamo wa Russia wa kuunga mkono madai ya Imarati
Dec 23, 2023 23:01Mkutano wa Sita wa Baraza la Ushirikiano la Nchi za Kiarabu na Russia ulifanyika tarehe 20 mwezi huu wa Disemba mwenyeji akiwa ni Nasser Burita Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco; na kwa mara nyingine tena katika taarifa ya mwisho ya mkutano huo Imarati ikatoa madai kuhusu visiwa vitatu vya Iran, yaliyoungwa mkono na Russia.
-
Azimio la Baraza la Usalama kuhusu Gaza: Ni hatua ya lazima lakini haitoshi
Dec 23, 2023 04:48Ijumaa ya jana, Desemba 22, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio la kuongeza misaada ya kibinadamu kwa watu wa Ukanda wa Gaza bila kutoa wito wa kusitishwa mapigano. Marekani na Russia, wanachama wawili wa kudumu wa Baraza la Usalama, hazikulipigia kura azimio hilo. Wajumbe wengine 13 wamelipigia kura ya ndiyo.