-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu juu ya ulazima wa mataifa ya Kiislamu kuwaunga mkono wananchi wa Gaza
Nov 06, 2023 02:51Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS), kwa mara nyingine tena ameshukuru na kusifu subira na muqawama wa wananchi wenye msimamo thabiti wa Gaza na kueleza masikitiko yake makubwa kwa jinai za utawala wa Kizayuni zinazofanywa kwa himaya na uungaji mkono wa moja kwa moja wa Marekani na baadhi ya nchi za Magharibi.
-
Hofu na wasiwasi wa Waisraeli kuhusiana na uwezekano wa kushtukizwa na Hizbullah
Nov 05, 2023 23:28Katika hali ambayo duru za Kizayuni bado zina wasiwasi kuhusu misimamo ya kimantiki na wakati huo huo isiyokuwa wazi ya Sayyid Hassan Nasrallah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon kuhusiana na matukio ya hivi karibuni ya nchi hiyo na Palestina, Ehud Barak, waziri mkuu wa zamani wa utawala huo ghasibu amesema Hassan Nasrallah ni mtu mwerevu sana na anaweza kuchukua hatua isiyotarajiwa ya kuishtukiza Israeli.
-
Safari ya ujumbe wa kiuchumi wa Afghanistan nchini Iran
Nov 05, 2023 06:20Ujumbe wa kiuchumi wa Afganistan umefanya safari nchini Iran kwa madhumuni ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara wa pande mbili.
-
Mpira wa kusimamisha au kupanua wigo wa vita Ghaza uko katika uwanja wa Netanyahu na jeshi la Kizayuni
Nov 05, 2023 03:22Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa inakaribia kufika mwezi mmoja tangu itekelezwe huku jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel likiendelea kuwaua watu wa Ghaza na kujaribu kufidia kushindwa kwao katika vita vya nchi kavu kwa kuwaua raia kwa umati.
-
Hitilafu kati ya Warepublican and White House kuhusu msaada kwa Israel na Ukraine
Nov 04, 2023 22:55Katika hali ambayo serikali ya Biden imetangaza kuunga mkono kikamilifu jinai za utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Ghaza na hata kupinga usitishaji vita, lakini suala la msaada wa kifedha kwa Israel ambalo linatiliwa maanani na Warepublican sambamba na mtazamo wa White ambayo inataka kutolewa kwa wakati mmoja misaada ya fedha na silaha kwa Ukraine limezusha hitilafu kubwa kati ya Kongresi na White House.
-
Kushtadi mashambulizi ya kigaidi huko Pakistan; sababu na taathira zake
Nov 04, 2023 08:12Kitengo cha Mahusiano ya Umma cha Jeshi la Pakistan kimetangaza kuwa vikosi vya jeshi hilo vimesambaratisha shambulio la kigaidi la leo asubuhi katika kambi ya kikosi cha jeshi la anga katika mji wa Mianwali katika jimbo la Punjab. Wavamizi watatu wameuwa na magaidi kadhaa wamekimbia eneo la tukio.
-
Nukta muhimu katika hotuba ya Hassan Nasrullah kuhusu Kimbunga cha al-Aqsa
Nov 04, 2023 03:36Huku akikosoa vikali katika hotuba yake ya jana Ijumaa, kimya cha nchi za Kiarabu kuhusiana na jinai zinazotekelezwa na utawala ghasibu wa Israel unaokalia kwa mabavu Quds Tukufu, dhidi ya watu wa Gaza, Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon, amesisitiza kuwa operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa imetekelezwa kikamilifu na Wapalestina, kwa ajili ya taifa la Palestina na malengo yao matukufu.
-
Mpira wa kugeuzwa vita vya Ghaza kuwa vita vya kieneo uko katika uwanja wa Israeli na waungaji mkono wake wa Magharibi
Nov 03, 2023 22:56Katika siku ya 29 ya Vita vya Ghaza, maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza yakiwemo ya az-Zaitun, al-Karamah na Beit Hanoun yangali yanashambuliwa kinyama na utawala katili wa Israel.
-
Kuendelea jinai za Wazayuni dhidi ya raia wa Gaza kwa uungaji mkono wa wazi wa Marekani
Nov 03, 2023 04:45Ikiwa ni katika muendelezo wa mauaji ya raia yanayofanywa na utawala unaoikalia kwa mabavu Quds Tukufu, ndege za kivita za utawala huo hivi karibuni zilishambulia kwa mabomu kambi ya wakimbizi ya Jabalia iliyoko kaskazini mwa Ukanda wa Gaza na kuua kwa umati zaidi ya raia mia moja wa Palestina na kujeruhi wengine zaidi ya mia tatu.
-
Misimamo inayogongana ya White House na Biden kuhusu kusitishwa mapigano huko Ghaza
Nov 02, 2023 23:57Ikiwa zimepita takribani wiki 4 tangu kuanza operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na mashambulizi ya jinai ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa maelfu ya Wapalestina hususan watoto na wanawake, Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu na mshirika wa kistratijia wa utawala wa Kizayuni, bado inataka kuendelezwa mauaji ya umwagaji damu huko Ghaza.