-
Iran yashambulia kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Oman, Qatar na Bahrain, yafunga Lango Bahari la Hormuz
Jul 12, 2026 04:20Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo asubuhi vimetekeleza operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Qatar, Oman na Bahrain, ikiwa ni hatua ya kujibu mashambulizi endelevu ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
Mkuu wa Idara ya Mahakama Iran: Tutawaandama wahalifu wa vita wa Marekani na Israel
Jul 12, 2026 04:18Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran, Hujjatul Islam Gholam Hossein Mohseni Ejei, amesema kuwa chombo hicho kitaendeleza hatua za kisheria za kufuatilia uhalifu uliofanywa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watu wa Iran, akisisitiza kwamba wahusika wa uhalifu wa kivita lazima waadhibiwe na walazimishwe kulipa fidia.
-
Ayatullah Mojtaba Khamenei asifu ushiriki ‘wa kihistoria’ wa waumini katika mazishi, aapa kulipiza kisasi kwa Kiongozi Shahidi
Jul 11, 2026 12:01Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ametoa shukrani zake za dhati kwa mahudhurio “ya kustaajabisha, yenye kuvunja nguvu za adui na ya kihistoria” katika mazishi ya Kiongozi Shahidi, akisisitiza kuwa malipo ya kisasi dhidi ya “watenda jinai wauaji waliodhalilika” ni jambo la yakini.
-
Utawala wa Israeli wamzuia Mufti wa Palestina kuingia Msikiti wa al-Aqsa
Jul 11, 2026 11:59Utawala wa Kizayuni wa Israel umemzuia Mufti Mkuu wa Palestina kuingia katika uzio wa Msikiti wa al-Aqsa jijini Al Quds (Jerusalem) kwa muda wa wiki moja baada ya kumteka nyara, katika hatua nyingine inayolenga viongozi wa kidini wa Palestina.
-
Wanafunzi wa Iran washinda katika Olympiadi ya kimataifa ya hisabati ya China
Jul 11, 2026 11:57Makamu wa Rais wa Iran anayeshughulikia masuala ya sayansi na teknolojia amepongeza ufanisi wa timu ya taifa ya Olympiad ya Hisabati ya Iran baada ya kushinda nafasi ya kwanza katika Mashindano ya Kimataifa ya Hisabati ya China (IMSC) ya mwaka 2026. Mafanikio haya yameelezwa kuwa ni dhihirisho la uwezo wa Iran katika nyanja ya sayansi.
-
Iran yaonya: Mashambulizi dhidi ya miundombinu yetu yatajibiwa kikamilifu
Jul 11, 2026 04:45Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Zolqadr, ametoa onyo kali na la moja kwa moja katika ujumbe wake kupitia mtandao wa X siku ya Ijumaa, akijibu vitisho vilivyotolewa hivi karibuni na Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Iran yalaani vikali mashambulizi ya kigaidi nchini Pakistan
Jul 11, 2026 04:42Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya kigaidi yaliyotikisa mkoa wa kusini-magharibi mwa Pakistan wiki hii.
-
'Makubwa zaidi katika historia ya binadamu': Zaidi ya watu milioni 43 wameshiriki mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi nchini Iran, Iraq
Jul 11, 2026 03:09Makumi ya mamilioni ya Wairani na waumini kutoka nchi mbalimbali duniani waligeuza shughuli ya mazishi ya Kiongozi aliyeuawa shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, kuwa mkusanyiko mkubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa kwa ajili ya mazishi kote duniani.
-
Abu Torabifardi: Utaratibu wa makubaliano ni ahadi kwa ahadi
Jul 11, 2026 02:50Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo katika mji wa Tehran amesisitiza kuwa hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani haikuandaliwa kwa msingi wa kuuamini uongozi wa Marekani na kueleza kuwa: Mfumo wa makubaliano hayo ni 'ahadi kwa ahadi'; na tunatangaza wazi wazi kwamba Marekani hataruhusiwa kamwe kuingilia masuala ya Mlango Bahari wa Hormuz.
-
Kamanda mkuu wa Majeshi Iran asema wauaji wa Kiongozi Muadhamu watakabiliwa na adhabu
Jul 11, 2026 02:47Kamanda wa Makao Makuu ya Majeshi ya Iran maarufu kwa jina la Kamandi ya Khatamul-Anbiya (SAW) amesema wale waliohusika na mauaji ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, watakabiliwa na adhabu, akielezea mahudhurio makubwa ya watu katika mazishi yake kuwa ni dhihirisho lenye nguvu la imani, ukakamavu na mshikamano.