-
IRGC yaitungua ndege ya kivita ya Marekani katika Ghuba ya Uajemi, yatoa onyo kali
May 27, 2026 03:24Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa vitengo vyake vya ulinzi wa anga vimetungua ndege ya kivita ya Marekani isiyo na rubani, aina ya MQ-9 Reaper, katika anga ya Ghuba ya Uajemi.
-
Iran yaonya kuwa, ikishambuliwa tena jibu la litakuwa ‘kali zaidi’ kuliko vita vilivyopita
May 27, 2026 03:16Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetoa onyo kali kuhusu mashambulizi ya kulipiza kisasi yatakayokuwa “mazito na makali zaidi” iwapo tawala za Marekani na Israel zitafanya uchokozi mpya.
-
Ujumbe wa Kiongozi Muadhamu- Siku ya Arafa
May 26, 2026 13:32Katika ujumbe wake kwa mnasaba wa kuwadia msimu wa Hijja ya Nabii Ibrahim (as), Ayatullah Seyyed Mojtaba Hosseini Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, ametaja amali na thikri zilizajaa maana za Hijja na kusema ni ishara za kudumu milele kwa wanadamu kwa ajili ya kuwahamasisha waelekee kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kuwa huru kutokana na minyororo ya Shetani na wafuasi wake, na wakati huo huo kufanya bidii bila kuchoka kwa ajili ya kuondokana na matamanio ya nafsi, na kufikia sa
-
Ujumbe wa Hija: Kiongozi Muadhamu ayatolea wito mataifa ya Kiislamu kuunda utaratibu mpya wa kikanda; asema enzi ya US imefikia tamati
May 26, 2026 11:24Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amezitolea wito nchi za Kiislamu kuzidisha ushirikiano na kuanzisha utaratibu mpya wa kieneo na kimataifa mbali na utawala wa Marekani.
-
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa: Iran haitasalimu amri wala kurudi nyuma
May 26, 2026 11:17Katibu wa Baraza Kuu la Usalama la Taifa la Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu "haitarudi nyuma" huku kukiwa na ripoti juu ya uwezekano wa kufikiwa makubaliano kati ya Tehran na Washington.
-
Baqaei: Marekani imefanya uhalifu wa kivita kwa kujaribu nguvu ya kombora lilitumika kwa mara ya kwanza kuua watu Lamerd, Iran
May 26, 2026 11:14Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: "Marekani ilitumia kwa mara ya kwanza kombora la PrMS katika shambulio lake kwenye eneo la makazi ya raia na uwanja wa michezo wa Lamerd katika Mkoa wa Fars kusini mwa Iran, kwa lengo la kujaribu nguvu za uharibifu za silaha hiyo."
-
Baqaei: Marekani inapasa kudhamini ushiriki wa timu ya taifa ya Iran katika mashindano ya Kombe la Dunia
May 26, 2026 02:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amezungumzia uvumi unaoendelea kuhusu kushiriki wa timu ya taifa ya kandanda ya Iran katika Kombe la Dunia la FIFA la 2026, na kusisitiza kuwa Marekani inawajibika kuandaa mazingira yanayofaa kwa timu hiyo kushiriki katika mashindano bila vizuizi vyovyote.
-
Pezeshkian: Iran haitasalimu amri kwa matakwa 'ya kupitiliza' ya Marekani, inataka kurejeshea haki zake kikamilifu
May 25, 2026 12:28Rais Masoud Pezeshkian ametangaza kwamba Iran haitasalimu amri kwa mashinikizo ya Marekani na matwaka ya kuchupa mipaka ya utawala huo, akisema wapatanishi wa Iran watahakikisha haki za taifa zinarejeshwa kikamilifu kupitia mchakato wa kidiplomasia.
-
Kiongozi wa machafuko yaliyofadhiliwa na Marekani mwezi Januari auawa nchini Iran
May 25, 2026 10:18Mahakama ya Iran imetangaza kwamba mmoja wa viongozi wa makundi yenye silaha yaliyohusika na ghasia zilizofadhiliwa na madola ya kigeni mnamo Januari 2026 amenyongwa katika mji wa Nain.
-
Pezeshkian: Iran iko tayari kuihakikishia dunia kwamba haifuatilii silaha za nyuklia
May 25, 2026 09:19Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kuihakikishia jamii ya kimataifa kwamba haifuatilii silaha za nyuklia.