-
Ujumbe wa Kiongozi Muadhamu Mpya wa Iran
Mar 13, 2026 12:44Ayatullah Sayyid Mojtaba Husseini Khamenei, Kiongozi mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe wake wa kwanza kulihutubia taifa la Iran.
-
Mamilioni ya Wairani washiriki maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds licha ya kudondoshewa mabomu na US, Israel
Mar 13, 2026 06:36Mamilioni ya wananchi wa Iran katika pembe zote za nchi wameshiriki katika maandamano makubwa ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds Ijumaa, huku tawala za kitwaghuti za Marekani na Israel zikiendelea kushambulia kwa mabomu miji mbali mbali ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Rais wa Iran asisitiza ulazima wa kusitishwa mara moja uvamizi wa Marekani na utawala wa Kizayuni
Mar 13, 2026 04:27Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, ameishukuru serikali na wananchi wa India kwa kuonesha mshikamano na watu wa Iran, akisema kuwa Iran daima imekuwa ikiiheshimu India kama rafiki na mshirika muhimu wa kiuchumi.
-
IRGC yashambulia meli nyingine ya mafuta ya US Ghuba ya Uajemi
Mar 13, 2026 03:57Kikosi cha Majini cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran IRGC kimetangaza habari ya kushambulia meli nyingine ya mafuta Marekani katika Ghuba ya Uajemi.
-
Larijani: Asia Magharibi itatumbukia gizani US ikishambulia mtandao wa umeme wa Iran
Mar 13, 2026 03:29Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ametoa onyo kali akijibu vitisho vipya vilivyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu kushambulia giridi ya taifa ya umeme wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mlango-Bahari wa Hormuz uendelee kufungwa; apongeza mchango wa wananchi
Mar 12, 2026 11:22Kiongozi wa tatu wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran leo ametoa ujumbe wake wa kwanza baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo akitilia mkazo umuhimu wa mchango wa wananchi na mahudhurio yao katika medani na kusema: Wananchi wanataka kuendelezwa mapambano athirifu na ya kumjutisha adui.
-
Jeshi Iran lashambulia makao ya Shin Bet na vituo vya ndege za kivita Israel
Mar 12, 2026 06:02Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu limetangaza kutekeleza shambulio la droni au ndege ya kivita isiyo na rubani dhidi ya kituo cha kijeshi cha Palmachim pamoja na makao ya Shin Bet ndani ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Rais wa Iran atangaza masharti ya kusitishwa vita vya kutwishwa vya US, Israel
Mar 12, 2026 03:51Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian ametangaza masharti kadhaa ya kuhitimisha vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu; huku tawala mbili hizo za kigaidi zikiendelea kushambulia maeneo muhimu ya kiraia kama shule, hospitali, makazi ya watu, na turathi za kihistoria za nchi hii.
-
Araghchi aonya UN: Kunyamazia kimya uvamizi wa US, Israel kutashadidisha taharuki katika eneo
Mar 12, 2026 03:23Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kuwa, kufumbia macho au kutochukua hatua za maana mkabala wa vitendo vya kivamizi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kutafungua njia ya kushadidi ukosefu wa utulivu na taharuki katika eneo.
-
Iran yasema haitashiriki Kombe la Dunia la FIFA 2026
Mar 12, 2026 02:57Waziri wa Michezo wa Iran, Ahmad Donyamali amesema timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kiislamu haitashiriki katika fainali za Kombe la Dunia katika msimu ujao wa joto, licha ya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Gianni Infantino kusisitiza kuwa amehakikishiwa na Rais Donald Trump wa Marekani kwamba Iran inakaribishwa kushiriki mashindano hayo makubwa zaidi ya soka duniani, pamoja na vita vinavyoendelea.