-
Rezaei: Iran itajiondoa katika mkataba wa kuzuia silaha za nyuklia iwapo itashambuliwa tena
May 25, 2026 09:18Iran imetoa onyo kali kwa Marekani, ikisema kuwa itajiondoa kwenye Mkataba wa Kuzuia Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT), ikiwa Marekani itaanzisha tena mashambulizi dhidi ya yake.
-
Rais Pezeshkian: Iran inapigania haki zake halali katika mazungumzo na Marekani
May 24, 2026 12:50Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa Iran inataka kurejesha haki zake halali katika mazungumzo na Marekani. Hata hivyo, ameeleza kuwa uzoefu mchungu wa majadiliano ya huko nyuma na Washington unaifanya Tehran kusonga mbele kwa tahadhari kubwa.
-
Iran yaonya: Tuko tayari kutoa jibu “la maangamizi” dhidi ya uchokozi mpya
May 24, 2026 12:40Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yako katika kiwango cha juu kabisa cha utayari na yataitoa “adhabu yenye maangamizi na ya kuzimu” iwapo adui ataanzisha tena vita au shambulio lolote la kichokozi dhidi ya nchi.
-
Qalibaf: Iran haina imani na Marekani, haitasalimu amri kuhusu haki zake
May 24, 2026 03:30Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Iran haina imani yoyote na Marekani na kwamba haitarudi nyuma kamwe katika kutetea haki zake za kitaifa wakati wa mazungumzo na Marekani yanayolenga kuhitimisha vita katika eneo lote la Asia Magharibi.
-
Jeshi la Iran lasema meli 25 zimepita katika Lango la Hormuz
May 24, 2026 03:28Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimetangaza kuwa meli 25, zikiwemo meli za mafuta, meli za mizigo (kontena), na meli zingine kibiashara, zimevuka Lango la Bahari la Hormuz katika kipindi cha saa 24 zilizopita hadi kufikia jana, baada ya kupata idhini na chini ya uratibu wa kiusalama wa jeshi hilo.
-
Balozi wa Iran UN apinga madai ya Marekani kuhusu shambulio dhidi ya kinu cha nyuklia cha UAE
May 24, 2026 03:26Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa ameyatupilia mbali madai ya Marekani kuhusu shambulio la ndege zisizo na rubani (drone) dhidi ya kinu cha kuzalisha umeme kwa nishati ya nyuklia cha Barakah nchini Falme za Kiarabu (UAE). Amesema kuwa Washington imetumia vibaya Baraza la Usalama ili kusambaza tuhuma za uongo dhidi ya Iran na mpango wake wa nyuklia wenye malengo ya amani.
-
Mkuu wa jeshi la Pakistan azungumza kwa kina na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran mjini Tehran
May 23, 2026 12:35Asim Munir, Mkuu wa jeshi la Pakistan amefanya mazungumzo ya muda mrefu na Waziri wa Mambo ya Nje Abbas Araqchi mjini Tehran, huku jitihada za kidiplomasia zikishika kasi ili kuzuia kushtadi hali ya mgogoro katika Asia Magharibi.
-
Iran yaiambia UN: Nchi za Ghuba ya Uajemi zinapasa kutoa jibu na kulipa fidia kwa mchango wao katika vita vya Marekani na Israel
May 23, 2026 12:32Amir Saeid Iravani Balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa nchi za kusini mwa Ghuba ya Uajemi na Jordan zinabeba dhima ya kuzisaidia Marekani na Israel katika uvamizi wao dhidi ya Iran.
-
Kamanda Talaei-Nik: Trump hana chaguo ila kukubali haki ya Iran
May 23, 2026 12:29Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Iran amesema: "Kushindwa adui kufungamana na matakwa halali ya taifa la Iran kutasababisha gharama kubwa na kushindwa zaidi adui Mzayuni na Marekani."
-
Rais Pezeshkian awataka wataalamu wa mahusiano ya umma kuvunja vikwazo vya vyombo vya habari vya Kizayuni
May 23, 2026 03:05Rais Masoud Pezeshkian anasema wataalamu wa mahusiano ya umma wanapaswa kuchukua jukumu muhimu katika kuongeza uelewa wa umma, ikizingatiwa kwamba vyombo vya habari vya Kizayuni vinawazuia watu kuona na kujua ukweli.