-
Baqaei: Kuharibiwa Taasisi ya Pasteur ya Iran ni tishio kwa usalama wa afya wa kikanda
May 23, 2026 02:41Ismail Baqaei, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amechapisha nukuu ya ripoti ya jarida la masuala ya tiba la The Lancet kuhusu uharibifu uliosababishwa na mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye Taasisi ya Pasteur ya Iran, na kusisitiza kwamba kuharibiwa taasisi hiyo ni tishio kwa usalama wa kikanda.
-
Imam wa Swala ya Ijumaa Tehran: Maadui watakabiliana na makombora mapya ikiwa watafanya makosa
May 22, 2026 15:05Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema: "Iwapo maadui watafanya kosa jingine, watakabiliana na vita vipana zaidi badala ya vita vya kikanda, na badala ya kuzuiliwa Mlango-Bahari wa Hormuz, wakati huo Mlango Bahari wa Bab al-Mandeb pia atafungwa.
-
Pezeshkian: Serikali imejitolea kikamilifu kuboresha uwezo wa Jeshi la Iran
May 22, 2026 06:55Rais Masoud Pezeshkian amesema serikali yake itatumia “nguvu na rasilimali zote zilizopo” kuimarisha majeshi ya ulinzi huku akisifu majibu ya kijeshi ya Iran kuwa “makini, madhubuti na yanayozuia uchokozi” kufuatia mashambulizi ya hivi karibuni yaliyotekelezwa na tawala za Marekani na Israel.
-
Jenerali Qa'ani: Freedom Flotilla imewafedhehesha Wazayuni
May 22, 2026 04:29Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema katika ujumbe wake kwamba mafanikio ya msafara wa meli za misaada ya kibinadamu kwa ajili ya watu wa Ukanda wa Gaza "Global Sumud Flotilla, yanaendelea.
-
“Tutawafanya maadui wajute”: Qalibaf aonya dhidi ya njama za Marekani kuanzisha vita vipya
May 21, 2026 13:24Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa onyo kali akisema kuwa mienendo ya wazi na ya siri ya adui inaashiria wazi kuwa wanapanga kuanzisha duru nyingine ya vita.
-
Kiongozi Muadhamu amkumbuka Shahidi Rais Raeisi, ampongeza kwa uwajibikaji
May 21, 2026 04:42Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ametoa ujumbe wa kuadhimisha mwaka wa pili tangu kufa shahidi aliyekuwa Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Ebrahim Raeisi. Katika ujumbe huo, alimwelezea marehemu Rais Raeisi kama kiongozi aliyekuwa na hisia ya juu ya uwajibikaji, mwenye kuzingatia uadilifu, mwenye kuendesha diplomasia hai na yenye manufaa, na hasa aliyekuwa karibu na wananchi kwa unyenyekevu na huruma.
-
IRGC yaonya kuwa vita vipya dhidi ya Iran vitavuka mipaka ya eneo
May 21, 2026 04:40Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetoa onyo kali kwamba endapo vita dhidi ya Iran vitaanzishwa tena, basi vita vya kikanda vilivyoahidiwa hapo awali safari hii vitapanuka kuvuka eneo la Asia Magharibi, na kwamba mapigo mazito yataelekezwa kutoka maeneo ambayo adui hawezi kuyadhania.
-
Iran yakosoa upotoshaji wa CENTICOM kuhusu mauaji ya halaiki ya Minab
May 21, 2026 04:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekadhibisha matamshi ya Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) kuhusu mashambulizi ya ya makombora yaliyofanywa katika shule ya msingi ya Shajareh Tayyebeh huko Minab kusini mwa Iran na kuyataja kuwa "yasiyo na msingi".
-
Kiongozi Muadhamu: Nguvu inayojitokeza ya Iran inahusiana moja kwa moja na ongezeko la idadi ya watu
May 20, 2026 11:12Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema kupanda hadhi ya Iran ya kuwa taifa kubwa na lenye taathira kunahusiana moja kwa moja na ongezeko la idadi ya watu wake, na kutoa wito wa kuzidishwa juhudi za kukuza utamaduni wa kuzaa watoto.
-
Mkuu wa vyombo vya mahakama: Shahidi Raisi alijitolea kuwatumikia wananchi
May 20, 2026 11:09Mkuu wa vyombo vya Mahakama vya Iran anasema kuwa Rais Shahidi Ebrahim Raisi alijitolea kwa dhati kuwatumikia wananchi na kusabilia maisha yake kwa ajili ya Iran.