-
Taifa Lamuaga kwa Hamasa Kiongozi Shahidi: Dhihirisho la Nguvu na Umoja Dhidi ya Maadui
Jul 05, 2026 10:46Huku taifa la Iran likimuaga kwa hamasa Kiongozi wake wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi, tukio hili limeakisi wazi na kwa mara nyingine mandhari ya kuvutia ya umoja, kusimama imara, na mwamko wa kina wa Umma wa Kiislamu.
-
Mamilioni wauswalia mwili wa Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei mjini Tehran
Jul 05, 2026 07:15Mamilioni ua waombolezaji wameshikiri Swala ya maiti ya mwili mtakatifu wa Imam shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, pamoja na kundi la wanafamilia wake watukufu iliyofanyika kwa uwepo mkubwa wa viongozi wa serikali, jeshi na umma kwa ujumla.
-
Rais Pezeshkian: Utawala wa Kizayuni ndio chanzo kikuu cha migogoro na ukosefu wa utulivu Asia Magharibi
Jul 05, 2026 03:50Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya mashambulizi dhidi ya nchi kadhaa za eneo la Asia Magharibi na umekuwa chanzo cha migogoro mingi pamoja na hali ya ukosefu wa usalama, huku akibainisha kwamba, nchi za Kiislamu hazijawahi kuanzisha mashambulizi ya aina hiyo.
-
Wizara ya Usalama ya Iran yaahidi kulipiza kisasi ajili ya damu ya Kiongozi aliyeuawa shahidi
Jul 05, 2026 03:49Wizara ya Usalama ya Iran imeapa kulipiza kisasi damu ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei, ikisisitiza kuwa mioyo iliyojeruhiwa ya wananchi wa Iran na wapenda uhuru duniani kote haitapata faraja yoyote isipokuwa kwa kulipiza kisasi dhidi ya wahusika.
-
Watu 6 wenye mfungamano na mitandao ya adui watiwa mbaroni Tehran
Jul 05, 2026 03:44Askari usalama wa mji wa Tehran wamewatia baroni watu sita waliokuwa wakifanya kazi katika mitandao ya maadui na dhidi ya mapinduzi. Mamluki hao walitiwa mbaroni katika eneo la Pardis, mashariki mwa mkoa wa Tehran.
-
Mamilioni wajitokeza Tehran kutoa heshima zao za mwisho kwa Kiongozi Shahidi Khamenei
Jul 04, 2026 11:45Mamilioni ya watu leo wamejitokeza katika Musalla wa Imam Khomeini mjini Tehran na kutoa heshima zao za mwisho kwa Kiongozi Shahidi Imam Khamenei aliyeuawa shahidi Februari 28 mwaka huu katika mashambulio ya kinyama ya Marekani na utawala haramuu wa Israel.
-
Mazishi ya Kiongozi Shahidi Khamenei yagongwa vichwa vya habari ulimwenguni
Jul 04, 2026 11:43Vyombo vya habari kama vile mashirika ya habari, vituo vya televisheni na magazeti ya kimataifa vimeonyesha umuhimu mkubwa kwa hafla ya mazishi ya Imam shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, ambapo tukio hilo limewekwa katika nafasi ya juu ya habari za kimataifa kwa kuripotiwa kwa karibu na kwa kina.
-
Mtafiti wa Russia: Iran imara urithi wa kimkakati wa Ayatullah Seyed Ali Khamenei
Jul 04, 2026 11:26Mtafiti mwandamizi wa Kituo cha Utafiti wa Asia Magharibi katika Taasisi ya Uchumi wa Dunia na Mahusiano ya Kimataifa ya Primakov ya Russia anaamini kuwa: Moja ya vipengele muhimu zaidi katika urithi wa kimkakati wa Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni kuanzishwa kwa mfumo wa kisiasa unaoweza kustahimili shinikizo la nje.
-
Spika Qalibaf amwambia Trump ashughulie lishe duni ya Wamarekani milioni 40
Jul 04, 2026 10:56Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amejibu bwabwaja za Rais Donald Trump dhidi ya wananchi wa Iran kwa kusisitiza kuwa, shughulikia utapiamlo wa watu milioni 40 nchini Marekani, na usihamishie matatizo yako kwa wengine.
-
Qalibaf ageuza diplomasia ya mazishi kuwa jukwaa la shughuli za kikanda
Jul 04, 2026 09:55Marasimu ya mazishi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi, Ayatollah Seyyed Ali Khamenei, yamekuwa zaidi ya shughuli ya maombolezo ya kitaifa. Mazishi haya yameipa Iran fursa kubwa ya kidiplomasia, huku viongozi wakuu na jumbe za ngazi za juu kutoka kote Asia na Mashariki ya Kati wakikusanyika mjini Tehran kwa ajili ya kujadili masuala ya usalama wa kikanda, diplomasia ya baada ya vita na ushirikiano wa kimkakati.