-
Viongozi wa dunia wafika Tehran kutoa heshima kwa Kiongozi Shahidi
Jul 04, 2026 04:28Viongozi waandamizi wa Iran, marais na wakuu wa nchi, pamoja na wageni mashuhuri na wajumbe wa ngazi za juu kutoka mataifa mbalimbali duniani, wamefika Tehran kutoa heshima zao kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei.
-
Marekani ilitekeleza kampeni ya kuzuia mataifa kuhudhuria mazishi ya Shahidi Ayatullah Khamenei
Jul 04, 2026 04:23Wakati huohuo, imebainika kuwa maafisa wakuu wa Marekani waliendesha kampeni kali katika siku tano zilizopita, wakijaribu kuyazuia mataifa kushiriki katika hafla za mazishi ya Ayatullah Khamenei.
-
Mufti wa Russia: Kiongozi shahidi wa Iran alifanya juhudi kubwa za kuleta umoja wa madhehebu ya Kiislamu
Jul 04, 2026 04:20Mufti na Mwenyekiti wa Baraza la Kidini la Waislamu wa Russia anaamini kuwa Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, kiongozi shahidi wa Iran, wakati wa uhai wake alichukua hatua kubwa katika kuimarisha umoja na maelewano kati ya madhehebu ya Kiislamu.
-
Spika Qalibaf: Kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya Iran na China ni jambo la dharura
Jul 04, 2026 04:15Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kimkakati, kisiasa na kibunge kati ya Tehran na Beijing.
-
Iran yaapa kulipiza kisasi kwa Kiongozi Shahidi huku wageni maalum wakimiminika kwa ajili ya mazishi
Jul 03, 2026 11:35Rais wa Iran na Spika wa Bunge wametoa kauli tofauti wakiahidi kuwajibisha tawala katili za Marekani na Israel kwa mauaji ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei, huku maafisa wa ngazi za juu kutoka zaidi ya nchi 30 wakikusanyika Tehran kwa ajili ya shughuli za mazishi zinazotarajiwa kuvutia hadi waombolezaji milioni 20.
-
Kwa nini Iran inafungamanisha mazungumzo ya amani na usitishaji kamili wa mapigano nchini Lebanon
Jul 03, 2026 11:11Katika hali ya sasa ya mgogoro wa Mashariki ya Kati, suala la Lebanon limeibuka kama moja ya mihimili mikuu na muhimu katika mazungumzo ya kidiplomasia na vyombo vya habari. Katika uwanja huu, sisitizo la Iran la kusitishwa kikamilifu uvamizi wa utawala haramu wa Israel nchini Lebanon kama sharti la mazungumzo na Washington limeibua maswali mengi miongoni mwa wachambuzi wa kikanda na kimataifa. Msimamo huu sio hitajio la kimkakati tu bali ni sehemu ya mantiki pana ya kimkakati ya sera za kigeni
-
Mamilioni wanatarajiwa shughuli ya kumuaga Kiongozi Shahidi nchini Iraq
Jul 03, 2026 07:24Mamilioni ya waumini wanatarajiwa kufurika katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala nchini Iraq kushiriki katika shughuli za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei.
-
Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu yaanza Tehran
Jul 03, 2026 06:35Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeanza awamu ya kwanza ya taratibu za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei, huku viongozi wa kimataifa na wanazuoni wa kidini wakifika katika Ukumbi wa Sala wa Imam Khomeini maarufu kama Mosalla mjini Tehran kutoa heshima zao za mwisho.
-
Pezeshkian: Mahudhurio makubwa katika mazishi ya Kiongozi Shahidi ni ‘jibu madhubuti’ kwa ubeberu na ugaidi
Jul 03, 2026 03:51Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa umati mkubwa wa wananchi utakaojitokeza katika shughuli ya mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, utakuwa “jibu madhubuti” dhidi ya vitendo vya kigaidi, ukatili na mbinu za kibeberu. Amesema kuwa tukio hilo litakuwa dhihirisho la wazi la umoja wa taifa la Iran na dhamira yake isiyotetereka katika kulinda uhuru na heshima ya nchi.
-
Onyo kali la Majeshi ya Iran: Uchokozi wa Marekani katika Lango la Hormuz utajibiwa haraka
Jul 03, 2026 03:45Kamandi Kuu ya Majeshi ya Iran, maarufu kama Kamandi ya Khatam al-Anbiya, imetoa onyo kali kuwa, uingiliaji wowote wa kijeshi wa Marekani katika Lango Bahari la Hormuz utajibiwa kwa kasi na maamuzi madhubuti na vikosi vya ulinzi vya Iran, huku ikisisitiza kuwa njia hiyo muhimu ya bahari iko chini ya mamlaka kamili ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.