-
Pezeshkian: Mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya viwanja vya michezo yafichua uadui kwa heshima ya Iran
May 15, 2026 06:06Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa kulengwa kwa viwanja vya michezo na miundombinu ya umma na Marekani pamoja na Israel wakati wa vita vya uchokozi kumefichua uadui wa washambuliaji hao dhidi ya heshima, furaha na fahari ya taifa la Iran.
-
Araghchi: UAE ni “mshirika hai” katika uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
May 15, 2026 06:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, ameikosoa vikali Falme za Kiarabu (UAE) kwa kuwa mshirika wa moja kwa moja katika uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran. Ametoa kauli hiyo akijibu madai yasiyo na msingi yaliyotolewa na mwakilishi wa UAE.
-
Araqchi katika mkutano wa BRICS New Delhi: Ushawishi wa Marekani unapungua
May 14, 2026 10:27Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi amesema kuwa wananchi wa Iran "wamesimama kidete na kwa fahari " dhidi ya machafuko ya kutisha, na kamwe hawatasalimu amri mbele ya matakwa ya Marekani nchi ambayo ushawishi wake duniani unazidi kupungua.
-
Vyombo vya Habari vya Marekani: Iran bado ina uwezo mkubwa wa makombora
May 14, 2026 08:43Kinyume na madai ya maafisa wa serikali ya Marekani wanaochochea vita, akiwemo Rais Donald Trump, vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti, vikinukuu tathmini za siri, kwamba Iran bado ina uwezo mkubwa wa makombora.
-
Jeshi la Iran: Hakuna silaha za Marekani zikazovuka Mlango-Bahari wa Hormuz
May 14, 2026 03:35Jeshi la Iran limetangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitaruhusu tena silaha za Marekani kuvuka Mlango-Bahari wa Hormuz na kuingia katika vituo vya nchi za kanda hii. Limesema kuwa njia hiyo ya kistratejia ya majini sasa iko chini ya udhibiti wa kimkakati wa vikosi vya ulinzi vya Iran.
-
Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Uko Imara Zaidi ya Ulivyokuwa Huko Nyuma
May 13, 2026 13:11Waziri Mkuu wa zamani wa Qatar ameeleza katika mahojiano marefu aliyofanyiwa na televisheni ya Al Jazeera kwamba, Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran uko mara zaidi hivi sasa kuliko ulivyokuwa huko nyuma.
-
Wizara ya Ulinzi wa Iran: Kubalini haki za Iran au mkabiliwe na kipigo kingine cha kijeshi
May 13, 2026 12:21Wizara ya Ulinzi ya Iran imesema maadui, Marekani na Uzayuni, wanapaswa kukubali haki halali za taifa la Iran, au wasubiri kushindwa tena katika nyanja za kidiplomasia na katika uwanja wa vita.
-
Kushiriki UAE katika vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran ni 'haramu kabisa'
May 13, 2026 12:18Chuo Kikuu cha Kimataifa cha al-Mustafa kimetangaza kuwa ushiriki, uwezeshaji na ushirikiano wa UAE katika vita vya hivi karibuni vya Marekani na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Iran ni sawa na "kusaidia kambi ya ukafiri dhidi ya ndugu Waislamu" na hivyo, "kimsingi ni haramu."
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Msimamo wa Marekani ndio kikwazo kikuu kumaliza vita
May 13, 2026 02:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amesema kuwa msimamo wa Marekani wa kutaka masharti ya kupita kiasi pamoja na mienendo yake mingine inayodhoofisha juhudi za diplomasia ndiyo vizuizi vikuu vya kumaliza mzozo uliozuka kufuatia vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Spika Qalibaf: Majeshi ya Iran yako tayari kuwashitua wavamizi
May 12, 2026 09:13Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf, amesema kuwa majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu yako katika hali ya juu kabisa ya utayari wa kivita na yako tayari kutoa jibu kali, la haki na linalostahili dhidi ya aina yoyote ya uchokozi. Amewaonya maadui kwamba mikakati na maamuzi yenye makosa hayatazaa chochote isipokuwa maafa.