-
Qalibaf: Hakutakuwa na mazungumzo mapya na Marekani kabla ya kutekeleza ahadi zake
Jul 01, 2026 10:20Mkuu wa timu ya Iran ya mazungumzo na Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaingia katika mazungumzo yoyote mapya na Marekani mpaka masharti yote yaliyomo katika hati ya makubaliano ya maelewano iliyopo yatakapotekelezwa kikamilifu.
-
Iran yasafirisha mapipa milioni 50 ya mafuta baada ya kuondolewa vikwazo vya Marekani
Jul 01, 2026 10:17Kufuatia kupunguzwa kwa vikwazo vilivyokuwa vinaikabili sekta ya mafuta, Iran imesafirisha takriban mapipa milioni 50 ya mafuta katika kipindi cha wiki mbili zilizopita, na inakadiriwa kuwa imepata mapato yanayozidi dola bilioni 3.5 za Kimarekani.
-
Mataifa zaidi ya 90 kuwakilishwa katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Jul 01, 2026 03:41Dunia inashuhudia mshikamano wa kipekee kufuatia taarifa kwamba wawakilishi kutoka nchi zaidi ya 90, pamoja na viongozi wa kidini, wasomi, na watu mashuhuri kutoka kila pembe ya dunia, wanatarajiwa kushiriki katika shughuli za mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyed Ali Khamenei.
-
Baghaei: Iran inafuatilia hatua kwa hatua utekelezaji wa Marekani wa MoU
Jul 01, 2026 03:40Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Tehran itafuatilia, dakika kwa dakika, iwapo Marekani itazingatia makubaliano ya maelewano (MoU) ya kumaliza vita, na akaonya kwamba Jamhuri ya Kiislamu haitatekeleza wajibu wake chini ya makubaliano hayo ikiwa ni upande mmoja pekee unaoyatekeleza.
-
Waziri: Iran itajibu ukiukaji wowote wa usitishaji vita
Jul 01, 2026 03:31Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hakiuna shaka yoyote kwamba, Tehran itajibu kwa nguvu zote ukiukaji wowote ule wa usitishaji vita.
-
Rais Pezeshkian asema Iran itatekeleza mapatano ikiwa Marekani itafanya hivyo
Jun 30, 2026 11:31Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kuwa makubaliano yoyote kati ya Iran na Marekani lazima yajikite katika heshima ya pande zote na ahadi za pamoja, na si kwa kutumia vitisho au shinikizo la upande mmoja.
-
Jeshi: Mazishi ya Kiongozi Shahidi yatakuwa mwamko wa kimataifa dhidi ya ugaidi na jinai za Marekani na Uzayuni
Jun 30, 2026 11:23Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limesema kuwa sherehe za kitaifa za kuaga na mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, zitatumika kama jukwaa la harakati za kimataifa za kulaani ugaidi na maandamano hai dhidi ya jinai zinazofanywa na mhimili wa Marekani na Uzayuni.
-
Pezeshkian: Dola bilioni 6 za Iran zinazozuiwa Qatar kuachiliwa
Jun 30, 2026 03:51Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, ametangaza kuwa kiasi cha dola bilioni 6 mali ya nchi hii zinazozuiliwa Qatar kufuatia mashinikizo ya Marekani, zitaachiliwa.
-
Wasomi wanawake wa Iran wataka Marekani na Israel ziwajibishwe kwa jinai zao
Jun 30, 2026 03:27Kundi la wanazuoni wanawake wa Iran, wasomi wa taaluma mbalimbali na wataalamu wa masuala ya utamaduni, limesambaza barua ya wazi likirekodi ukiukaji wa kimfumo uliofanywa na Marekani na Israel wakati wa vita vya hivi karibuni dhidi ya Iran, na limetoa wito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua za dharura za uwajibikaji.
-
Kinyume na propaganda za adui, sekta ya ulinzi ya Iran inaendelea kupata mafanikio: Naibu Mkuu wa Jeshi
Jun 29, 2026 12:29Kamanda wa Jeshi la Iran amesema Jamhuri ya Kislamu imepata mafanikio endelevu katika teknolojia ya ulinzi wa ndege zisizo na rubani na anga licha ya madai ya uhasama ya vyombo vya habari.