-
Wanafunzi 185 wameuawa shahidi Iran katika hujuma za kigaidi za Israel, Marekani
Mar 04, 2026 02:23Waziri wa Elimu Iran, Alireza Kazemi, amesema katika mashambulizi ya kigaidi yaliyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran Jumamosi, hadi sasa wanafunzi wasiopungua 185 wameuawa shahidi.
-
IRGC: Hakuna jinai na mauaji ya kidhulma yanayofanywa na US na wazayuni yatayopita bila ya jibu
Mar 03, 2026 15:49Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesisitiza kuwa, wahalifu wa Kimarekani na Kizayuni wajue kwamba hakuna hata moja kati ya jinai na mauaji ya kidhulma wanayofanya yatakayopita bila ya jibu.
-
IRGC: Majibu yajayo yatakuwa makali zaidi, Tel Aviv yateketea kwa makombora
Mar 03, 2026 14:06Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema, kiwango cha nguvu za makombora kitaongezwa na mwendelezo wa mashambulio dhidi ya maadui wavamizi utazidi kurefushwa.
-
George Galloway: Minab ndio mauaji makubwa zaidi ya wanafunzi wasichana katika historia
Mar 03, 2026 09:11George Galloway, mbunge wa zamani wa Uingereza amesema mauaji ya halaiki yaliyofanywa na Marekani dhidi ya wasichana 167 waliokuwa na umri wa kati ya miaka 7 na 12 wakiwa madarasani katika Shule ya Msingi ya Minab nchini Iran ndio maafa makubwa zaidi yaliyowahi kufanywa na Marekani tangu wakati wa Vita vya Vietnam.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi: Tumeanza wimbi la 15 la Opesheni Ahadi ya Kweli-4 dhidi ya kambi za Marekani
Mar 03, 2026 07:23Wimbi la 15 la Operesheni Ahadi ya Kweli-4 limeanza kwa jina la msimbo la Yaa Zahra (AS) kwa mashambulizi mseto ya makombora, ndege za kivita zisizo na rubani na operesheni maalumu ya kikosi cha wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu dhidi ya kambi za jeshi la Marekani katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Araqchi: Iran haina uadui na nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi
Mar 03, 2026 07:21Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema jibu la Iran la kushambulia kambi za kijeshi za Marekani katika baadhi ya nchi za Ghuba ya Uajemi halina maana kwamba Iran inashambulia nchi hizo.
-
Makamanda wa ngazi za juu wa Iran wameuawa shahidi katika hujuma ya kigaidi ya Israel, Marekani
Mar 01, 2026 04:18Kundi la makamanda wa Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wameuawa shahidi katika hujuma ya kigaidi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Iran kutoa jibu kali kwa wauaji wa wanafunzi 150
Mar 01, 2026 03:58Viongozi wa Iran wamelaani vikali shambulio la anga la utawala katili wa Israel dhidi ya shule ya msingi ya wasichana katika mji wa Minab, ulioko katika mkoa wa Hormozgan, kusini mwa Iran, lililopelekea kuuawa shahidi wanafunzi zaidi ya 150.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameuawa shahidi katika hujuma ya kigaidi ya Marekani na Israel
Mar 01, 2026 03:15Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Raji’un. Kufuatia shambulio la kikatili na la kigaidi la utawala wa Kizayuni na Marekani, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ameuawa shahidi.
-
Spika wa Iran: Israel, US zimekanyaga mstari wetu mwekundu
Mar 01, 2026 03:07Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran), Mohammad Bagher Ghalibaf amesema Rais wa Marekani, Donald Trump na Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu wamevuka mstari mwekundu wa Jamhuri ya Kiislamu, na watalipa gharama kubwa kwa jinai hiyo.