-
Madai ya Uongo Kuhusu Kufikiwa Malengo ya Marekani katika Vita Dhidi ya Iran
Jun 27, 2026 05:20J.D Vance, Makamu wa Rais Donald Trump wa Marekani, amedai kuwa malengo yote yaliyotangazwa na utawala wa nchi hiyo na hasa ya kijeshi na ya nyuklia katika vita vyake vya kichokozi dhidi ya Iran yamefikiwa. Vance amedai kuwa Marekani imefanikiwa kufikia yale yote iliyokuwa imepanga kuyafikia kwa kutumia uwezo wake wa kiuchumi, kidiplomasia na kijeshi.
-
IRGC yashambulia ngome za jeshi la Marekani kulipiza kisasi shambulio dhidi ya maeneo ya pwani ya Iran
Jun 27, 2026 03:24Kikosi cha Wanamaji la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kimeshambulia ngome za kijeshi za Marekani katika eneo la Magharibi mwa Asia kulipiza kisasi uchokozi wa awali dhidi ya maeneo ya pwani ya Iran.
-
Majeshi ya Iran yaonya kuhusu jibu kwa tishio lolote la Israel
Jun 27, 2026 03:01Kamandi Kuu ya Majeshi ya Iran imeonya kwamba Jamhuri ya Kiislamu itajibu “hatua hatari” za Israel katika anga za baadhi ya nchi jirani.
-
Iran yalaani taarifa ya kichochezi ya nchi za Ghuba ya Uajemi na Marekani
Jun 27, 2026 02:53Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali taarifa ya pamoja ya Marekani na Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (P-GCC), ikiitaja kuwa ni “ya kuingilia mambo ya wengine, isiyo ya kuwajibika, na ya kichochezi,” huku ikizionya nchi za eneo hilo dhidi ya kuendelea kushirikiana kwa misimamo ya uadui na Washington.
-
Araqchi: Hatutasahau wala hatutasamehe mauaji ya Sayyidi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Jun 26, 2026 11:23Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika ujumbe wake kwamba: "Kuuliwa shahidi Sayyid na kinara wa mashahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu hakutasahaulika wala hakutasamehewa."
-
Iran: Waliohusika na mauaji ya wanafunzi wa shule ya Minab wachukuliwe hatua
Jun 26, 2026 04:21Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani "uhalifu mbaya" uliofanywa na Marekani katika shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh ya Minab nchini Iran wakati wa mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kislamu, na kutoa wito kwa wahusika wote, wapangaji na viongozi kuwajibishwa kikamilifu, akisisitiza kwamba: "Kumbukumbu ya watoto wa Minab inahitaji haki, uwajibikaji na utekelezaji, si kukaa kimya."
-
Rais Pezeshkian: Imam Hussein (a.s.) ametufundisha kusimama dhidi ya dhulma
Jun 25, 2026 10:07Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kuwa, Imam Hussein (a.s.) ametufundisha kusimama dhidi ya dhulma, vishawishi vya madaraka, na tamaa ya maslahi binafsi.
-
Baghaei: NATO inapaswa kuwajibishwa kwa kushiriki katika vita dhidi ya Iran
Jun 25, 2026 09:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwamba, Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) na nchi wanachama wake, zikiwemo Italia na Romania, ambazo Katibu Mkuu wa NATO amekiri waziwazi nafasi yao katika kutekeleza mashambulizi haramu na ya kihalifu dhidi ya Iran, zinapaswa kuwajibishwa kwa aina yoyote ya ushirikiano katika uhalifu uliofanywa na Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Iran yapendekeza kuanzishwa Umoja wa Redio na Televisheni wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai
Jun 25, 2026 04:22Mwakilishi wa Mkuu wa Kitengo cha Matangazo ya Ng'ambo ya Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ametoa pendekezo la kuanzishwa Umoja wa Redio na Televisheni wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai kama utaratibu mpya wa kuimarisha diplomasia ya vyombo vya habari na muungano wa kitamaduni miongoni mwa nchi wanachama.
-
Mamilioni ya Wairani washiriki maombolezo kuelekea siku ya Ashura
Jun 24, 2026 11:04Mamilioni ya Waislamu katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maeneo mengine ya dunia leo mchana wameshiriki katika maombolezo ya kumbukumbu ya Ta'asua na jioni hii wanashiriki katika hafla za mkesha wa Ashura ambayo ni kukumbuka siku ya kuuliwa shahidi mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW), Imam Hussein bin Ali bin Abi Twalib (AS).