-
Qaddoumi: Iran ina haki ya kujibu mashambulizi dhidi yake
Mar 15, 2026 08:41Mwakilishi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) Tehran amesisitiza kuwa Iran ina haki kamili na ya pande zote ya kukabiliana na mashambulizi ya adui kwa kila njia inayoiona inafaa.
-
Uvamizi Dhidi ya Iran na Nyufa Ndani ya Ikulu ya Marekani
Mar 15, 2026 08:38Taarifa mpya imefichua kuwa, makamu wa rais wa Marekani, J.D. Vance, tokea alikuwa na mashaka kuhusu vita dhidi ya Iran na hadi sasa anaendelea kupinga mitazamo ya Rais Trump kuhusu vita hivyo ambavyo viko katika wiki ya tatu sasa vimeigharimu Marekani mabilioni ya dola.
-
Jenerali Shekarchi: Tumeharibu kambi zote za US katika eneo, meli ya Abraham Lincoln imetimka
Mar 15, 2026 08:35Msemaji wa Vikosi vya Ulinzi vya Iran, Brigedia Jenerali Abolfazl Shekarchi amesema kambi za kijeshi za Marekani zilizoundwa kwa kutumia rasilimali za Waislamu kwa kisingizio cha kudhamini usalama wa eneo, huku zikifuja mali za mataifa ya Waislamu, zimeharibiwa katika mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Spika wa Iran: Kambi za kijeshi za US ni tishio kwa nchi wenyeji wake
Mar 15, 2026 08:34Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema Marekani imeitoa kafara kila nchi kwa maslahi ya utawala wa Kizayuni wa Israel, na kwamba kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi hazizipi ulinzi nchi wenyeji.
-
Ufaransa yamkaidi Trump, yasema manowari zake hazitashiriki katika vita dhidi ya Iran
Mar 15, 2026 08:09Wizara ya Ulinzi ya Ufaransa imetangaza katika taarifa rasmi kwamba manowari za nchi hiyo hazitashiriki katika operesheni yoyote ya mashambulizi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
IRGC: Kama Netanyahu hajafa tutaendelea kumuwinda na kumuua
Mar 15, 2026 08:08Idara ya Mawasiliano ya Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) imetangaza kuwa kama Waziri Mkuu mtendajinai wa Israel atakuwa hai jeshi hilo linamuwinda na kumuangamiza.
-
The Economist: Pipa la mafuta ya petroli litafikia dola 200
Mar 15, 2026 05:37Gazeti la masuala ya kiuchumi la The Economist limeripoti kuwa gharama ya pipa moja la mauta ya petroli itafikia dola 200 iwapo vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vitaendelea.
-
Netanyahu yuko wapi? Galloway ashangazwa na video yake ya Akili Mnemba
Mar 14, 2026 08:05Kiongozi wa Chama cha Wafanyakazi Uingereza, George Galloway amesema video ya hotuba ya Benjamin Netanyahu iliyotengezwa kwa kutumia Akili Mnemba (AI) inaibua masuali mengi kuhusu kitendawili cha aliko Waziri Mkuu huyo wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Shambulio Lailenga Rada na Mfumo wa Ulinzi wa Anga wa Ubalozi wa Marekani Baghdad
Mar 14, 2026 07:52Baada ya ubalozi wa Marekani mjini Baghdad nchini Iraq kulengwa kwa shambulio, vyanzo vya habari vimeripoti kuharibiwa kwa mfumo wa ulinzi wa anga wa ubalozi huo.
-
Maseneta wa Marekani wataka kufukuzwa Waziri wa Vita wa nchi hiyo kwa kuua wanafunzi shule ya msingi Minab
Mar 14, 2026 07:30Maseneta Elizabeth Warren na Chriss Van Hollen wa Marekani wametoa wito wa kutimuliwa Waziri wa Vita wa nchi hiyo, Pete Hegseth, kwa sababu ya kutenda jinai ya kuua watoto wadogo wa shule ya msingi nchini Iran.