-
Utafiti: Kilimo cha mihadarati ya afyuni nchini Afghanistan kimepungua kwa 20% katika mwaka 2025
Nov 07, 2025 06:47Utafiti mpya uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kupambana na Madawa ya Kulevya na Uhalifu UNODC umeonyesha kupungua kwa kiasi kikubwa kwa kilimo cha mmea wa afyuni (Opium) nchini Afghanistan katika mwaka huu wa 2025, hali inayoashiria mabadiliko makubwa katika uzalishaji na biashara ya mihadarati katika ukanda huo.
-
Jordan yalaani ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni Ukingo wa Magharibi
Nov 07, 2025 03:57Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jordan imetangaza kuwa, inalaani vikali uamuzi wa hivi karibuni wa utawala ghasibu wa Israel wa kutangaza zabuni ya ujenzi wa vitongoji vipya 356 vya walowezi wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.
-
Wanawake 400 wa Kipalestina na watoto wangali wanashikiliwa mateka na Israel
Nov 07, 2025 03:56Mashirika matatu ya Kipalestina yanayohusiana na masuala ya mateka yametangaza kuwa, utawala ghasibu wa Israel unawashikilia Wapalestina 9,250 wakiwemo wanawake 49 na watoto 350 katika jela zake.
-
Rais mzee zaidi duniani aapishwa kuongoza Cameroon kwa muhula wa nane
Nov 07, 2025 03:52Kiongozi wa muda mrefu wa Cameroon, Paul Biya, ameapishwa kwa muhula mpya wa miaka saba kufuatia ushindi wake katika uchaguzi wa rais wa mwezi uliopita, ambao mpinzani wake ameutaja kama "mapinduzi ya kikatiba".
-
Wanamgambo wa RSF waafiki pendekezo la kusitisha vita Sudan
Nov 07, 2025 03:38Vikosi vya Usaidizi wa Haraka vya Sudan (RSF) vimetangaza kwamba vinakubali usitishaji vita uliopendekezwa na Kamati ya Kimataifa ya Pande Nne.
-
Baghaei: Vikwazo vya Marekani dhidi ya Wairani ni jinai dhidi ya ubinadamu
Nov 07, 2025 03:24Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, vikwazo vya Marekani dhidi ya Wairani ni jinai dhidi ya ubinadamu.
-
Araghchi: Tunaendelea kufungua milango ya masoko ya kimataifa kwa Iran
Nov 07, 2025 00:17Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, wizara yake inaendelea na jitihada zake za kidiplomasia za kufungua milango ya masoko ya kimataifa kwa ajili ya Iran na kuwasahilishia mambo wale wote wanaojishughulisha na masuala ya kiuchumi.
-
Rwanda yashutumu ujumbe wa Umoja wa Mataifa kwa mafunzo ya jeshi la DRC
Nov 07, 2025 00:15Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Rwanda, amekosoa ujumbe wa kueneza amani wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (MONUSCO) kwa kutoa mafunzo kwa wanajeshi 120 wa DRC.
-
Ripoti ya kushtusha ya Umoja wa Mataifa; mauaji ya kimbari ya Wapalestina Ghaza yangali yanaendelea
Nov 06, 2025 23:17Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, mauaji ya kimbari ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza yangali yanaendelea.
-
Hizbullah: Hatutaki mazungumzo na Israel, hatutaki makubaliano nao
Nov 06, 2025 23:06Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imeandika barua ya wazi kuhusu mitego iliyowekwa na Wazayuni kupitia kile kinachodaiwa ni mazungumzo ya amani na kusema kuwa, lengo la mazungumzo hayo ni kulitwisha taifa la Lebanon siasa za upande mmoja za Israel na kuvunja nguvu mwamko wa wananchi wa Lebanon wa kupigania haki zao mbele ya adui mpenda vita. Imesema: Mapambano ndiyo yanayolifanya taifa kubaki kuwa na heshima.