-
'Bodi ya Amani' ya Trump ni aina ya ukoloni mamboleo
Jan 22, 2026 23:51Mkuu wa Jamaat-e-Islami Pakistan (JIP) ametangaza kwamba "Bodi ya Amani" iliyotangazwa na Rais wa Marekani, Donald Trump kusimamia utawala wa eneo la Palestina la Ukanda wa Gaza ni aina mpya ya mfumo wa ukoloni mamboleo. Bodi hiyo ni taasisi inayojumuisha watu kama Tony Blair, mmoja wa wahusika wakuu wa mauaji ya mamilioni ya watu wa Iraq.
-
Putin: Denmark imekuwa ikiitazama Greenland kama koloni lake
Jan 22, 2026 02:31Rais wa Russia, Vladimir Putin amesema, Denmark imekuwa ikiichukulia Greenland kama koloni lake. Amesema hayo akitoa mtazamo wake kuhusu mpango wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa 'kukinunua' kisiwa hicho cha Aktiki kinachojitawala.
-
Bunge la EU lasimamisha makubaliano ya biashara na US; kisa vitisho vya Trump
Jan 22, 2026 02:21Bunge la Ulaya limesimamisha rasmi mchakato wa kuidhinisha makubaliano yake ya kibiashara na Marekani, kutokana na vitisho vya Rais Donald Trump vya kutoza ushuru wa asilimia 10 kwa bidhaa za EU zinazoenda Marekani, iwapo umoja huo hautaafiki azma ya Washington ya kuitwaa Greenland.
-
Mahakama ya Kimataifa ya Jinai chini ya kivuli cha undumakuwili wa Marekani
Jan 22, 2026 00:56Naibu mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa ametishia kuichukulia hatua zaidi Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC iwapo itaendeleza uchunguzi wake kuhusu uhalifu na jinai za nchi hiyo.
-
"Haiwezi Tena Kuvumilika", asema Waziri Mkuu wa Ubelgiji akiitaka Ulaya iamue moja kuhusu Trump
Jan 21, 2026 07:09Waziri Mkuu wa Ubelgiji Bart De Wever amesema, ni lazima Ulaya imueleze wazi Rais wa Marekani Donald Trump kwamba hali ilipofikia hivi sasa "Haiwezi Tena Kuvumilika".
-
Zilzala ya kisiasa yatishia Kombe la Dunia 2026... Ujerumani yadokeza kususia au kufutwa mashindano hayo
Jan 21, 2026 04:17Mashindano ya Kombe la Dunia 2026, yaliyopangwa kufanyika msimu ujao wa joto Amerika Kaskazini, yanakabiliwa na tishio lisilo la kawaida, baada ya sauti nyingi nchini Ujerumani kuibuka zikitaka kususiwa Kombe la Dunia la mpira wa miguu," na hata kutoa wito wa kufutwa kabisa mashindano hayo ili kupinga sera za Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Gazeti la New York Times laorodhesha "uongo" wa Rais Trump katika mwaka mzima
Jan 21, 2026 04:15Gazeti la New York Times linaamini kwamba katika mwaka wa kwanza wa muhula wake wa pili, Rais wa Marekani Donald Trump amesema uongo mwingi, kutoa madai yasiyo na msingi na upotoshaji ili kuhalalisha mabadiliko na kudanganya kuhusu mafanikio katika maeneo ya uchumi, uhamiaji na kadhalika.
-
Russia yasisitizia tena haki ya Iran ya kunufaika na nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani
Jan 20, 2026 23:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov amesisitizia tena haki ya Iran ya kutumia nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani.
-
Trump atishia kuiwekea Ufaransa ushuru wa 200% kumshinikiza Macron ajiunge na 'Bodi ya Ghaza'
Jan 20, 2026 23:08Rais wa Marekani Donald Trump amemkosoa vikali Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa kukataa kujiunga na kile kinachoitwa "Bodi ya Amani" ya Washington kwa ajili ya Ghaza, huku mpango huo ukikabiliwa na ukosoaji mkubwa wa wataalamu wa sheria za kimataifa wanaouelezea kuwa ni upanuzi wa ukaliaji wa mabavu wa eneo hilo la Palestina unaofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Mchambuzi wa tiba wa CNN: Mpimeni Trump uzima wa akili
Jan 20, 2026 23:04Kufuatia vituko alivyofanya hivi karibuni Donald Trump kwa barua aliyomwandikia Waziri Mkuu wa Norway, Dk. Jonathan Reiner tabibu na mhadhiri katika Chuo Kikuu cha George Washington ametaka rais huyo wa Marekani apimwe uzima wa akili.