-
Vyombo vya habari vyafichua nafasi ya Ufaransa katika mauaji ya kimbari ya Rwanda
Oct 26, 2018 08:15Vyombo vya habari vimefichua picha za video zinazoonesha waziwazi nafasi ya Ufaransa katika mauaji ya kimbari yaliyofanyika Rwanda mwaka 1994.
-
Sudan yaondoa marufuku ya uingizaji mazao ya kilimo kutoka Misri
Oct 26, 2018 08:11Rais Omar al Bashir wa Sudan jana alitoa dikrii na kuondoa marufuku ya miezi 17 ya kuzuia kuingizwa nchini humo mazao ya kilimo kutoka Misri.
-
Mazungumzo ya kusaka amani ya Burundi yaahirishwa
Oct 25, 2018 14:00Shughuli za ufunguzi wa mazungumzo ya amani ya Burundi zilizokuwa zifanyike jana Jumatano mjini Arusha kaskazini mwa Tanzania zililazimika kusogezwa mbele ingawa msimamizi wa mazungumzo hayo Rais wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa hakueleza sababu.
-
Umoja wa Mataifa waonya kuhusu kuendelea mauaji ya umati dhidi ya Waislamu wa Rohingya
Oct 25, 2018 14:00Mkuu wa Wachunguzi Maalumu na Timu ya Kutafuta Ukweli ya Umoja wa Mataifa nchini Myanmar ameonya juu ya kuendelea mauaji ya umati dhidi ya Waislamu wa jamii ya Rohingya nchini humo.
-
Ethiopia yapata rais wa kwanza mwanamke
Oct 25, 2018 13:55Bunge la Ethiopia limemuidhinisha mwandiplomasia wa kimataifa, Sahle-Work Zewde kuwa rais wa kwanza mwanamke wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Mripuko wa bomu Sinai, Misri waua wafanyakazi watatu
Oct 25, 2018 13:52Wafanyakazi watatu raia wa Misri wameuawa katika shambulizi la bomu lililotokea leo Alkhamisi katika eneo linalokumbwa na misukosuko na ukosefu wa usalama la Rasi ya Sinai, kaskazini mwa nchi hiyo.
-
Makundi ya waasi Jamhuri ya Afrika ya Kati yatia saini makubaliano ya amani
Oct 25, 2018 13:29Makundi matano ya waasi ya kaskazini magharibi mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati yametia saini makubaliano ya amani.
-
Uchunguzi: Mlipuko wa Ebola magharibi mwa Afrika umesababisha hasara ya dola bilioni 53
Oct 25, 2018 02:34Virusi vya Ebola vilivyozikumba nchi za magharibi mwa Afrika hususan Sierra Leone, Guinea and Liberia mwaka 2014 vilisababisha hasara inayokadiriwa kufikia dola bilioni 53.
-
UN: Pande hasimu Sudan Kusini ziliwateka nyara na kuwanajisi mamia ya wanawake
Oct 24, 2018 16:49Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini umeeleza kuwa, askari wa serikali na waasi nchini humo wamewateka nyara mamia ya wanawake na wasichana mwaka huu na wengi miongoni mwao walibakwa na kufanywa watumwa wa ngono.
-
Watu zaidi ya 50 wauawa katika mapigano baina ya koo huko Somaliland, Somalia
Oct 24, 2018 16:31Mapigano yaliyojiri kati ya koo hasimu katika kijiji cha Dhumey eneo la Somaliland lililojitenga na Somalia yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 50.