Jeshi la Majini la Iran kupata meli tatu mpya za kivita
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i77822-jeshi_la_majini_la_iran_kupata_meli_tatu_mpya_za_kivita
Kamanda wa Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema jeshi hilo hivi karibuni litapokea meli tatu mpya za kivita ambazo ziktakuwa katika bahari za kaskazini na kusini mwa nchi.
(last modified 2026-07-03T11:45:53+00:00 )
Dec 09, 2021 04:44 UTC
  • Jeshi la Majini la Iran kupata meli tatu mpya za kivita

Kamanda wa Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema jeshi hilo hivi karibuni litapokea meli tatu mpya za kivita ambazo ziktakuwa katika bahari za kaskazini na kusini mwa nchi.

Akizungumza Jumatano, Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran Admeri Shahram Irani amesema jeshi hilo lina mipango maalumu ya kitaifa na kimataifa.

Admeri Irani amesema Jeshi la Majini la Iran lina mkakati  wa kuhakikisha kuwa zana zake zote za kivita  za maeneo ya kaskazini na kusini mwa nchi ni mpya. Aidha amesema kwa mujibu wa mpango uliopo uundwaji meli mpya za kivita na zana zinginezo utafanyika ndani ya nchi kutegemea wataalamu Wairani.

Kamanda wa Jeshi la Majini la Iran Admeri Shahram Irani

Amongeza kuwa manoari ya Damavand itatumwa upande wa kaskazini mwa nchi katika Bahari ya Kaspi na meli zingine mbili za kivita zitatumwa upande wa kkusini mwa nchi katika Ghuba ya Uajemi ikiwemo meli ya kukusanya taarifa za siri yenye uwezo wa kusheheni helikopta. Halikadhalika amesema nyambizi mpia pia inatazamiwa kuanza kutumika katika Ghuba ya Uajemi.

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasisitiza kuwa uwezo wake mkubwa wa kijeshi si tishio kwa nchi jirani bali uwezo huo unadhamini usalama wake na wa eneo.