-
Iran na Qatar zasisitiza kuzuiwa mashambulio ya Israel dhidi ya miundomsingi ya Syria
Dec 12, 2024 07:38Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Qatar wamesisitiza juu ya ulazima wa kufanyika juhudi na kuchukuliwa hatua za dhati ili kusimamisha mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya miundomsingi ya Syria na kukalia kwa mabavu maeneo zaidi ya nchi hiyo na utawala huo ghasibu.
-
Vyombo vya Magharibi vyaakisi kwa wingi miongozo ya Kiongozi Muadhamu
Dec 12, 2024 03:01Mashirika ya habari ya nchi za Magharibi yameakisi kwa wingi hotuba na miongozo muhimu ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei aliyotoa jana Jumatano akisisitiza kuwa Marekani na utawala wa Kizayuni ni wahusika wakuu wa matukio ya Syria.
-
Iran yailaani Daesh (ISIS) kwa kumuua waziri wa serikali Taliban Afghanistan
Dec 12, 2024 02:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mauaji ya Khalil-ur-Rehman Haqqani, waziri wa masuala ya wakimbizi wa serikali ya kundi la Taliban nchini Afghanistan.
-
Ndege ya mizigo iliyotengenezwa Iran yafanyiwa majaribio
Dec 12, 2024 00:55Ndege nyepesi ya mizigo ya Iran, iliyopewa jina la Simorgh, ambayo imeundwa kikamilifu na wataalamu wa Kampuni ya Utengenezaji Ndege ya Iran (HESA), imefanyiwa majaribio yaliyofana, baada ya kufanyiwa ukaguzi mbalimbali ili kupokea cheti cha kuraka.
-
Hotuba ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kuhusu sababu za kuanguka utawala wa Syria
Dec 11, 2024 23:50Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amehutubia hadhara ya matabaka tofauti ya wananchi akigusia matukio ya hivi sasa ya Syria na eneo la Magharibi mwa Asia kwa ujumla, na kueleza sababu za kuanguka utawala wa Syria pamoja na mikakati ya Iran katika kukabiliana na hali ya sasa.
-
Imamu Khamenei: Kilichotokea Syria ni matokeo ya mpango wa pamoja wa Marekani na Israel
Dec 11, 2024 09:07Kiiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, kiilichotokkea Syria ni njama na mpango wa pamoja wa Marekani na utawala haramu wa Israel.
-
Ayatullah Jannati: Marekani na washirika wake lazima wawajibike kuhusu Syria
Dec 11, 2024 09:07Katibu wa Baraza la Kulinda Katiba ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani na waitifaki wake wanapaswa kuwajibishwa kuhusiana na matukio ya Syria.
-
Baqaei: Iran inahuisha sentrifyuji zaidi za kisasa katika fremu ya NPT
Dec 11, 2024 03:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa uamuzi wa karibuni wa Tehran wa kuhuisha sentrifyuji zaidi za kisiasa umechukuliwa katika fremu ya haki ya nchi wanachama wa mkataba wa NPT na kwa kutolewa taarifa kabla na kwa usimamizi wa Wakala wa kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Meja Salami: Iran inafuatilia kwa nguvu zote kuiangusha Israel; nguvu zake haziathiriwi na hali ya Syria
Dec 10, 2024 08:35Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema Iran inafuatilia kwa nguvu zote kuuangusha utawala wa Kizayuni unaoukalia ardhi kwa mabavu na akasisitiza kuwa, vikosi vya ulinzi vya Iran vimeyaweka kwenye nukta ya kuyalenga shabaha maslahi ya kistratejia na muhimu ya maadui katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Mkuu wa Vyuo vya Kidini akutana na Maulamaa wa Kisunni wa Kurdistan ya Iran, atilia mkazo umoja
Dec 10, 2024 08:34Mkuu wa Vyuo vya Kidini nchini Iran Ayatullah Alireza A'arafi amesisitizia umuhimu wa umoja baina ya nchi za Kiislamu na akasema: kwa kuzingatia hali ya eneo, kujenga umma mmoja na kuwepo umoja baina ya Waislamu ni jambo muhimu zaidi sasa hivi kuliko wakati mwingine wowote.