-
Maelfu waandamana Australia kupinga ziara ya rais wa utawala wa Israel
Feb 11, 2026 03:32Ziara rasmi ya rais wa utawala wa Israel, Isaac Herzog, nchini Australia ilikumbwa na maandamano makubwa siku ya Jumatatu, huku maelfu ya waandamanaji wakijitokeza katika miji kadhaa, hali iliyopelekea kuwepo makabiliano na polisi.
-
Reuters: Kuna kambi ya siri ya wapiganaji wa RSF nchini Ethiopia
Feb 11, 2026 03:28Ripoti ya shirika la habari la Reuters, iliyotokana na picha za satalaiti na ushuhuda rasmi, imefichua kuwepo "kambi ya siri" nchini Ethiopia kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa maelfu ya wapiganaji wa Rapid Support Forces (RSF), ambao wanapigana na jeshi nchini Sudan.
-
Mgombea ugavana wa Republican huko Florida: Ukuta wa Kuomboleza huko Israel ni ukuta wa kijinga
Feb 11, 2026 03:26Mgombea wa chama cha Republican katika nafasi ya gavana wa Florida, James Fishbach, amezua mzozo wa kisiasa baada ya shambulio lake la moja kwa moja dhidi ya Ukuta wa Magharibi (Wailing Wall) na ahadi yake ya kukata uhusiano wote wa kiuchumi na Israel kama atashinda kiti hicho.
-
Ramaphosa na Putin wajadili suala la kuhitimisha vita kati ya Russia na Ukraine
Feb 11, 2026 03:25Rais wa Vladimir Putin wa Russia amefanya mazungumzo ya simu na mwenzake wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa ambapo pande hizo mbili zimejadili kuhusu suluhu inyoweza kufikiwa nchini Ukraine.
-
Macron: Utawala wa Trump una uadui na Umoja wa Ulaya na unataka kuuvunja
Feb 11, 2026 03:25Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, amesema kwamba utawala wa Rais wa Marekani, Donald Trump unaonyesha uadui dhidi ya Umoja wa Ulaya na unataka kuuvunja.
-
Iran yaonya kuhusu njama za Israel huku ikiendeleza mazungumzo ya kidiplomasia na Marekani
Feb 10, 2026 23:37Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ametoa tahadhari kuhusu azma ya utawala wa Israel ya kuishawishi Marekani iingie katika vita vingine dhidi ya Iran, wakati mazungumzo mapya ya nyuklia kati ya Tehran na Washington yakiwa yameanza.
-
Mpango wa hatua nne wa Netanyahu wa kuumeza Ukingo wa Magharibi
Feb 10, 2026 22:52Uamuzi wa baraza la mawaziri la Benjamin Netanyahu siku ya Jumapili kuhusu Ukingo wa Magharibi ulikuwa msumari wa mwisho katika jeneza la udanganyifu na matumaini ya wale waliofikiri kwamba chini ya kivuli cha makubaliano na wavamizi wa Kizayuni, inawezekana kupata haki za Wapalestina.
-
Maadhimisho ya Mapinduzi ya Kiislamu: Maandamano kufanyika katika miji 1,400, waandishi habari 7,700 wanaakisi tukio hilo
Feb 10, 2026 11:41Sherehe na maandamano ya kuadhimisha miaka 47 ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yatafanyika katika miji zaidi ya 1,400 nchini kote, huku waandishi wa habari wa ndani na nje wapatao 7,700 wakitarajiwa kuripoti matukio hayo.
-
Milio mikali ya risasi yasikika karibu na gereza la Conakry, mji mkuu wa Guinea
Feb 10, 2026 11:38Duru za habari zimearifu kuwa ulinzi mkali umeimarishwa baada ya milio mikali ya risasi kusikika mapema leo karibu na gereza kuu katika mji mkuu wa Guinea, Conakry.
-
Kamanda wa ngazi ya juu wa al Shabaab auawa katika oparesheni ya usalama Somalia
Feb 10, 2026 11:32Idara ya Intelijinsia na Usalama wa Taifa ya Somalia (NISA) leo Jumanne imetangaza kuuawa kiongozi wa ngazi ya juu wa wanamgambo wa kundi la al- Shabaab katika oparesheni ya usalama.