-
Larijani akutana na Sultani wa Oman, mazungumzo baina ya wawili yaendelea kwa saa tatu
Feb 10, 2026 10:48Akiendelea na mashauriano yake ya kikanda, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili Muscat mapema leo akiongoza ujumbe wa ngazi za juu na kufanya mazungumzo na Mfalme Haitham bin Tariq katika mkutano ulioendelea kwa karibu saa tatu.
-
Umoja wa Afrika watoa wito wa kusitishwa vita nchini DRC
Feb 10, 2026 10:31Rais wa Angola na wawakilishi kadhaa wa Umoja wa Afrika wametoa wito wa kusitishwa mapigano nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya mkutano na Rais Felix Tshisekedi.
-
Kusimama kidete Somalia dhidi ya mpango hatari wa Wazayuni huko Somaliland
Feb 10, 2026 09:25Somalia imeuonya utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu kuwahamisha kwa lazima wa Wapalestina na kuwapeleka Somaliland ambalo limejitangazia uhuru.
-
Rais Pezeshkian: Iran haitaki vita; mashinikizo ya kiuchumi yanalenga kuichafua serikali
Feb 10, 2026 03:52Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza tena msimamo wa Iran wa kuunga mkono amani, akisema kuwa nchi hii haijawahi kutaka kuanzisha vita, licha ya kukabiliwa na uhasama wa wazi kutoka kwa maadui zake.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani mradi mpya wa Israel wa kunyakua maeneo ya Ukingo wa Magharibi
Feb 10, 2026 03:51Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonyesha wasiwasi mkubwa na kulaani uamuzi wa hivi karibuni wa Israel wa kuidhinisha hatua zinazorahisisha upanuzi wa makaazi ya walowezi wa Kizayuni na kupanua udhibiti wa kiutawala na utekelezaji wa sheria wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa.
-
Iran inaweza kupunguza kiwango cha urutubishaji urani iwapo ‘vikwazo vyote vitaondolewa’
Feb 10, 2026 03:46Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) amesema kuwa uwezekano wowote wa kupunguza kiwango cha urutubishaji wa urani ambayo sasa ni imefika hadi asilimia 60 utategemea kikamilifu iwapo vikwazo vyote dhidi ya nchi hiyo vitaondolewa.
-
Türk: Janga la haki za binadamu Sudan linaweza kuzuilika
Feb 10, 2026 03:46Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu, Volker Türk, ameliambia Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kwamba machafuko ya El Fasher, Sudan, ni “janga kubwa la haki za binadamu linaloweza kuzuilika,” kufuatia miezi ya kuzingirwa na njaa iliyochochewa na kundi la waasi la RSF.
-
Msemaji wa Majeshi: Iran haitasalimu amri mbele ya mashinikizo ya Marekani wakati wa mazungumzo
Feb 10, 2026 03:42Iran haitasalimu amri wala kukubali mashinikizo au masharti ya Marekani huku ikiendelea na mazungumzo na Washington, amesema Brigedia Jenerali Abolfazl Shekarchi, msemaji wa Vikosi vya Ulinzi vya Iran, katika mahojiano maalum na Press TV.
-
Lavrov: Kadhia ya Epstein imedhihirisha sura halisi ya 'kuabudu shetani' ya watu mashuhuri wa Magharibi
Feb 09, 2026 23:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergey Lavrov amesema, mtindo mchafu wa maisha wa mfadhili na mhalifu wa vitendo vya ngono wa Marekani Jeffrey Epstein pamoja na tapo lake ni ushuhuda wa kuporomoka kimaadili shakhsia muhimu na maarufu wa Magharibi.
-
Kuungana makundi ya Kipalestina dhidi ya njama za utawala wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi
Feb 09, 2026 23:03Makundi ya mapambano ya ukombozi ya Palestina yamesisitiza ulazima wa kukabiliana na mipango ya Wazayuni wenye misimamo mikali katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.