-
Jeshi la Israel lashambulia hospitali, skuli na 'maeneo salama' Ghaza na kuua watu 50
Dec 23, 2024 03:52Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel linaendelea kufanya mashambulio ya kinyama katika Ukanda wa Ghaza na kuwaua shahidi Wapalestina wengine wasiopungua 50 katika kipindi cha 24 zilizopita.
-
Mjumbe wa Ansarullah: Utawala wa Kizayuni hauna ubavu wa kukabiliana na vikosi vyetu peke yake
Dec 23, 2024 02:20Mjumbe Mwandamizi wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesisitiza kwa kusema: "mashambulizi yetu yaliukanganya mfumo wa ulinzi wa anga wa Marekani na kupelekea kutunguliwa ndege ya kivita ya Marekani kwa shambulio lao wenyewe" na akaongeza kuwa utawala wa Kizayuni hauna ubavu wa kukabiliana na Wayemen peke yake na ndio maana unaomba msaada kwa watu wanaouunga mkono.
-
Jeshi la Yemen lathibitisha kudungua ndege ya kivita ya Marekani aina ya F-18
Dec 22, 2024 23:42Jeshi la Yemen linasema kuwa limefanikiwa kuzuia shambulio la pamoja la Marekani na Uingereza kwa kuiangusha ndege ya kivita ya kisasa ya Marekani aina ya F-18 na kulazimisha ndege za maadui kuondoka katika anga ya Yemen.
-
Shirikisho la Soka la Palestina: Wanamichezo 644 wameuawa shahidi tangu kuanza vita vya Gaza
Dec 22, 2024 23:40Shirikisho la Soka la Palestina limetangaza kuwa, wanamichezo 644 wameuawa shahidi tangu utawala haramu wa Israel ulipoanzisha hujuma na mashambulio ya kinyama dhidi ya Gaza Oktoba mwakka jana.
-
Jeshi la Israel lashambulia shule na hospitali huko Gaza na kuua raia 8
Dec 22, 2024 09:23Jeshi katili la Israel limefanya mashambulizi mapya kwenye vituo vya kiraia kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, na kuua na kujeruhi Wapalestina kadhaa katika eneo hilo lililozingirwa
-
Ndege ya kivita ya Marekani yadunguliwa kwenye Bahari Nyekundu ikivamia Yemen
Dec 22, 2024 09:19Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) imesema ndege yake ya kivita imedunguliwa kwenye Bahari Nyekundu katika kile ilichodai kuwa ni shambulizi la kimakosa kutoka jeshi lenyewe la Marekani, ikiwa katika operesheni yake dhidi ya Yemen kwa lengo la kuuunga mkono utawala wa Israel
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Yemen azionya nchi za Magharibi zinazoiunga mkono Israel
Dec 22, 2024 09:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Yemen amelaani hujuma za hivi karibuni za anga zilizotekelezwa na jeshi la Marekani huko Sana’a na kusisitiza kwamba, nchi yoyote inayounga mkono uchokozi wa utawala wa Kizayuni wa Israel ni mshirika katika jinai za utawala huo
-
Balozi wa Yemen Tehran: Wayemen wamevuruga uchumi wa utawala wa Kizayuni kwa mashambulizi yao
Dec 22, 2024 04:40Balozi wa Yemen mjini Tehran, Iran, amesema kuwa wananchi wa Yemen wamefanikiwa kuvuruga uchumi wa utawala wa Kizayuni kwa kutekeleza oparesheni zao za kijeshi katika Bahari Nyekundu dhidi ya utawala huo; na hasa uchumi wa bandari ya Ailat ambayo ni bandari kubwa zaidi ya utawala wa Kizayuni ambayo imetangaza kufilisika.
-
Maandamano dhidi ya al Jolani yaanza Syria
Dec 22, 2024 04:24Duru za habari zimeripoti kuwa kutekwa nyara raia wa Syria katika mkoa wa Halab nchini humo kumezushha cheche za awali za maandamano na malalamiko dhidi ya Muhammad al Jolani kamanda wa kundi la upinzani lenye silaha la Hay'at Tahrir al Sham(HTS).
-
Hamas yaendeleza juhudi za kufikia mapatano ya kusitisha vita Ukanda wa Gaza
Dec 22, 2024 04:19Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palstina (Hamas) imeripoti kuwa makundi ya muqawama ya Palestina yamekutana katika kikao cha pamoja huko Cairo, Misri na kwamba upo uwezekano wa kufikia mapatano ya kusitisha vita huko Ukanda wa Gaza.