-
CNN: Trump amezitishia au kuzishambulia nchi 15 akiwa madarakani
May 29, 2026 03:05Ripoti ya televisheni ya CNN imeeleza kuwa Rais Donald Trump wa Marekani amezitishia, ameeleza wazi uwezekano wa kufanya mashambulizi au amezishambulia nchi 15 katika mihula yake miwili ya uongozi; yaani kwa mahesabu ya haraka amefanya hivyo kwa nchi moja kati ya kila nchi 13 duniani.
-
Marekani yarejesha vikwazo dhidi ya Ripota Maalumu wa UN kwa kufichua mauaji ya kimbari ya Israel
May 28, 2026 10:40Marekani imemuwekea tena vikwazo Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu kwa sababu tu ya kufichua mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Russia yaunga mkono msukumo wa Afrika wa kudai fidia kutoka kwa madola ya kikoloni
May 27, 2026 03:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov, amesema nchi yake inaunga mkono msukumo wa Afrika wa kutaka fidia kutoka kwa madola ya kikoloni. Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha Siku ya Afrika mjini Moscow, Lavrov amesema suala hilo ni sehemu ya mapambano mapana dhidi ya ukoloni mambo-leo.
-
Mahujaji wanasimama Arafa leo kutekeleza nguzo muhimu ya Hija
May 26, 2026 03:17Mamilioni ya Mahujaji wa Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu, Al Kaaba, leo wanasimama katika uwanja wa Arafa katika kilele cha ibada tukufu ya Hija.
-
Papa Leo aomba radhi kutokana na nafasi ya Kanisa Katoliki katika biashara ya utumwa ya kuvuka Bahari ya Atlantiki
May 26, 2026 03:04Katika hatua ya kihistoria, Papa Leo wa XIV Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani ameomba radhi kutokana nafasi ya Baraza Kuu la Uongozi wa Kanisa Katoliki na Vatican la kuhalalisha utumwa na kushindwa kulaani suala hilo kwa karne kadhaa.
-
John Mearsheimer: Hakuna nguvu duniani yenye uwezo wa kuishinda Iran
May 26, 2026 02:53Profesa wa sayansi ya siasa na mtaalamu wa nadharia ya mahusiano ya kimataifa amesema kuwa: Wakati Marekani na Israel zimeshindwa kuishinda Iran kwa kutumia nguvu zao zote, katika kipindi cha siku 40 za mashambulizi ya anga, hakuna nguvu nyingine duniani yenye uwezo wa kufanya hivyo.
-
Rais wa China aunga mkono diplomasia ya amani kati ya Iran na Marekani
May 26, 2026 02:50Katika kikao chake na Waziri Mkuu na Mkuu wa Majeshi wa Pakistan, Rais wa China amesisitiza uungaji mkono wa Beijing kwa upatanishi wa Islamabad na diplomasia inayoendelea katika eneo la Magharibi mwa Asia kwa ajili ya amani, akitolea mfano ziara ya hivi karibuni ya Asim Munir, Mkuu wa Majeshi wa Pakistan jijini Tehran.
-
El Baradei: Mwendawazimu Trump anatafuta njia ya kujiondoa kwenye vita dhidi ya Iran
May 25, 2026 09:13Mkuu wa zamani wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ametangaza kuwa mtu mmoja mwendawazimu alianzisha vita dhidi ya Iran na sasa anatafuta njia ya kujiondoa vitani.
-
Sababu za kuongezeka mgawanyiko barani Ulaya kuhusu utawala wa Kizayuni
May 24, 2026 06:54Mbali na maoni ya wananchi, baadhi ya wabunge wa Bunge la Ulaya pia wameutaka Umoja wa Ulaya uchukue hatua kali dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel na viongozi wake.
-
Sababu ya kujiuzulu Mkurugenzi wa Intelijensia ya Kitaifa wa Marekani
May 23, 2026 13:14Kuibuka kwa baadhi ya tofauti kati ya Rais wa Marekani na mkuu wa jumuiya ya ujasusi ya nchi hiyo kumezua shaka kuwa kujiuzulu kwa Tulsi Gabbard kulitokana na sababu za kisiasa.