-
CENTCOM: Wanajeshi wetu waliojeruhiwa katika vita dhidi ya Iran wamefika 290
Mar 25, 2026 07:49Kamandi Kuu ya jeshi gaidi la Marekani (CENTCOM) imetangaza kuwa karibu wanajeshi 290 wa nchi hiyo wamejeruhiwa katIka vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Jenerali wa Marekani: Wairani wanaweza kukabiliana na uchokozi wa Marekani na Israel kwa miaka mingi
Mar 25, 2026 07:30Jenerali mstaafu wa Marekani amezungumzia mashinikizo ya kiuchumi na kisiasa yanayoongezeka kwa serikali ya Washington kutokana na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran, na kukiri kwamba Wairani wanaweza "kukabiliana na mashambulizi haya kwa miaka mingi."
-
Waziri Mkuu wa Uhispania: Vita dhidi ya Iran ni janga na maafa makubwa
Mar 25, 2026 07:30Waziri Mkuu wa Uhispania ametangaza kwamba vita vya sasa vya Marekani na Wazayuni katika Mashariki ya Kati ni "vibaya zaidi" kuliko vita vya Iraq mwaka 2003 na ni "janga kubwa," na kusema: Utawala wa Kizayuni wa Israel unataka kurudia "uharibifu" uleule wa Gaza nchini Lebanon.
-
Wamarekani wakosoa sera za vita za Trump, wasema: Uhai wa wanajeshi umewekwa hatarini kwa sababu tu ya Israel
Mar 24, 2026 07:41Sauti za kupinga sera za vita za Rais Donald Trump zinaendelea kuongezeka nchini Marekani huku wananchi na familia za wanajeshi wanaotumwa Mashariki ya kati kwa ajili ya vita vya nchi hiyo na Irael dhidi ya Iran zikisema watoto wao wanauawa kwa maslahi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Mgogoro wa nishati waiathiri Ulaya; Slovenia mafuta yanatolewa kwa mgao
Mar 24, 2026 07:40Athari mbaya za vita vya Marekani na utawala ghasibu wa Israel zinaanza koenekana waziwazi barani Ulaya na kuathiri sekta mbalimbali za viwanda, usafirishaji na maisha ya watu wa kawaida.
-
Trump aondoa vitisho baada ya onyo kali kutoka Iran
Mar 24, 2026 04:34Rais wa Marekani amelazimika kuondoa vitisho vyake kuhusu kushambulia miundombinu ya umeme ya Iran baada ya onyo kali la Iran.
-
Waziri Mkuu wa Uhispania ataka kulindwa vyanzo vya nishati katika Mashariki ya Kati
Mar 23, 2026 07:09Waziri Mkuu wa Uhispania ametahadharisha kuhusu mgogoro wa nishati wa muda mrefu kwa wanadamu wote kutokana na vita vya uchokozi vya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran na kutaka kulindwa vyanzo vyote vya nishati katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Sauti na nara za kupinga vita dhidi ya Iran zasikika kuanzia Uhispania hadi Canada
Mar 23, 2026 06:59Wananchi wa Uhispania wameandamana kulaani vita vya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran. Maelfu ya wananchi wa Uhispania wamemiminika katika mji mkuu wa nchi hiyo, Madrid, kutangaza upinzani wao kwa vita vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran.
-
Marekani yajipapatua kudhibiti bei ya mafuta; Washington yafuta vikwazo vya mafuta ya Iran kwa muda
Mar 22, 2026 06:13Baada ya Iran kufunga Lango Bahari la Hormuz na kupanda bei ya nishati kwa kiwango kikubwa, Wizara ya Fedha ya Marekani imelazimika kutangaza kuwa imeondoa vikwazo vya kununua mafuta ya Iran kwa kipindi cha mwezi mmoja.
-
Rais Putin: Russia itaendelea kuwa rafiki na mshirika wa Iran
Mar 22, 2026 05:06Rais wa Russia amesisitiza kuwa nchi yake itaendelea kuwa mshirika mwaminifu wa Iran katika nyakati hizi ngumu za kukabiliana na hujuma ya kichokozi ya utawala wa Kizayuni na Marekani