Hujambo mpenzi msikilizaji na karibu tutupie jicho baadhi ya matukio makubwa ya michezo yaliyojiri ndani ya siku saba zilizopita, kitaifa, kieneo na kimataifa.
Huu ni mkusanyiko wa baadhi ya matukio makubwa ya spoti yaliyojiri ndani ya siku zilizopita, kitaifa, kieneo na kimataifa....
Manchester City ya Uingereza imeibuka kidedea na kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia kwa Klabu kwa mara ya kwanza, na hivyo kuidhihirishia dunia kwa mara nyingine tena kuwa ndiyo klabu bora zaidi duniani.
Timu ya taifa ya soka ya vijana ya Uganda imebuka kidedea baada ya kuichabanga Kenya mabao 2-1 katika fainali ya Mashindano ya Kandanda ya Kanda ya Afrika Mashariki na Kati Cecafa kwa vijana wenye chini ya miaka 18.
Kwa mara ya kwanza, Ujerumani imetwaa ubingwa wa Kombe la Dunia kwa vijana wa kiume wenye chini ya umri wa miaka 17.
Klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini imetwaa ubingwa wa Kombe la Ligi ya Kandanda ya Afrika baada ya kuicharaza Wydad Casablanca jumla wa mabao 3-2 kwenye fainali ya mkondo wa pili iliyopigwa Jumapili hii ya Novemba 12.
Mechi za raundi ya 1 ya Ligi ya Klabu Bingwa barani Asia zilifanyika jana Jumanne.
Timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitandika timu ya soka ya taifa ya Angola mabao 4 kwa sifuri katika mechi ya kirafiki iliyochezwa katika dimba la Azadi mjini Tehran.
Duru ya 12 ya Mashindano ya Vijana ya Taekwondo nchini Lebanon ilimalizika Jumatatu kwa timu ya mabinti ya Iran kutwaa taji la ubingwa wa Asia.
Timu ya soka ya Arsenal ya Uingereza jana iliendeleza matokeo mazuri ya msimu huu wa Ligi Kuu ya EPL baada ya kuwatandika watani wao wa jadi Manchester United mabao 3 kwa moja la kufutia machozi.