Sakata la uchaguzi wa Meya jijini Dar es Salaam, Tanzania + Sauti
Mar 06, 2016 14:39 UTC
Wakazi wa jiji la Dar es Salaam wameitaka mamlaka inayohusika kusimamia uchaguzi wa meya wa jiji hilo unaokwama kufanyika kutokana na kuahirishwa mara kwa mara, kutangaza tarehe rasmi ya kufanyika uchaguzi huo ili jiji hilo limpate kiongozi wake.
Kauli hizo za wananchi zinakuja baada ya mivutano kati ya vyama vikuu vya siasa nchini humo, umoja wa UKAWA na chama cha mapinduzi CCM vinavyodhani taratibu za uchaguzi huo zinavunjwa, jambo linalosababisha vurugu kila uchaguzi huo unapopangwa kifanyika, na mamlaka kuamua kuahirishwa kwake.
TAARIFA ZAIDI NA OMAR MANJI KUTOKA DAR….
Tags