-
Uchaguzi Uganda; Bobi Wine apinga ushindi wa Museveni
Jan 18, 2026 06:56Kiongozi wa upinzani na mshindani mkuu wa Rais Yoweri Museveni katika uchaguzi mkuu wa hivi karibuni nchini Uganda, Robert Kyangulani maarufu kama Bobi Wine amesema hakubaliani na matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo.
-
Watu wanane wafa, 20 wajeruhiwa, makumi ya nyumba zateketea kwa moto, Kibera nchini Kenya
Jan 18, 2026 02:16Taarifa za awali zinasema kuwa watu wasiopungua wanane wamepoteza maisha na wengine zaidi ya ishirini wamejeruhiwa baada ya moto mkubwa kuzuka katika eneo la Makina la makazi duni ya watu huko Kibera, Kaunti ya Nairobi nchini Kenya.
-
Doumbouya, kiongozi wa kijeshi aliyegombea urais na kushinda aapishwa kuwa rais wa Guinea
Jan 17, 2026 23:40Mamady Doumbouya, jenerali aliyeongoza jeshi la Guinea kuchukua madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi mnamo mwaka 2021, ameapishwa kuwa rais wa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.
-
Tume ya Uchaguzi Uganda: Yoweri Museveni ameshinda muhula wa saba wa urais
Jan 17, 2026 11:16Tume ya uchaguzi nchini Uganda imemtangaza Yoweri Kaguta Museveni kama mshindi wa Uchaguzi wa Rais uliofanyika Alhamisi wiki hii, akiwa na jumla ya kura 7,946,772 ambayo ni asilimia 71.65% ya kura zote zilozopigwa.
-
Chad yaelemewa na wakimbizi wa Sudan, CAR, Cameroon, Nigeria na kwengineko
Jan 17, 2026 04:40Mzigo mkubwa wa wakimbizi wanaomiminika kila leo nchini Chad umeielemea serikali ya nchi hiyo ambayo muda wote inaiomba jamii ya kimataifa na hasa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR liisaidie kubeba mzigo huo.
-
Makamanda wa Wanamaji wa China na Afrika Kusini watembelea meli za kivita za Iran mjini Cape Town
Jan 17, 2026 03:12Makamanda na wanajeshi wa majini ya China na Afrika Kusini wametembelea meli za kivita za kikosi cha majini cha Iran kilichotia nanga katika bandari ya Cape Town, pembeni mwa mazoezi makubwa ya kimataifa ya majini yanayoandaliwa na Afrika Kusini.
-
Hofu yatanda Afrika kuhusu utafiti wa chanjo unaofadhiliwa na Marekani kuhusu homa ya ini
Jan 17, 2026 03:09Utafiti wa chanjo uliogharamiwa na Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Marekani (CDC) nchini Guinea‑Bissau umekosolewa vikali na wataalamu wa afya pamoja na maafisa wa ndani ya taasisi hiyo, huku afisa mmoja wa CDC akiuulinganisha na jaribio maarufu la kaswende la Tuskegee.
-
UN yataka msaada wa haraka ufike Sudan kuepusha janga la kibinadamu
Jan 17, 2026 03:08Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa wakimbizi na Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, Barham Salih, ametoa wito wa dharura wa msaada wa kibinadamu na ulinzi kwa watu wanaokimbia vita vya kikatili nchini Sudan, akionya kuwa mgogoro huo sasa umekuwa janga kubwa zaidi na lenye athari mbaya zaidi la watu kufurushwa makwao duniani.
-
WFP: Mamilioni ya watu katika njaa kali Afrika Magharibi na Kati
Jan 16, 2026 23:22Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetoa onyo kali kutokea mjini Dakar, Senegal, likieleza kuwa bila rasilimali na hatua za haraka, watu walio katika mazingira magumu zaidi huko Afrika Magharibi na Kati wanakabiliwa na mwaka mwingine wa baa la njaa.
-
Zoezi la kuhesabu kura Uganda linaendelea, Museveni anaongoza kwa zaidi ya 76%
Jan 16, 2026 07:45Zoezi la kuhesabu kura nchini Uganda kufuatia uchaguzi mkuu uliofanyika Alkhamisi ya jana linaendelea huku matokeo ya awali yakionyesha kuwa, Yoweri Museveni rais wa sasa anaongoza kwa wingi wa kura.