-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran azungumza na mawaziri wenzake Qatar na Saudia kuhusu utulivu wa kieneo
Apr 27, 2026 09:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amefanya mazungumzo ya simu kwa nyakati tofauti siku ya Jumapili na mawaziri wenzake wa Qatar na Saudi Arabia, ikiwa ni sehemu ya juhudi pana za kidiplomasia za kukomesha mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran yasema Lango-Bahari La Hormuz liko wazi kwa Kenya
Apr 27, 2026 09:30Balozi wa Iran nchini Kenya, Dkt. Ali Gholampour, amesema kuwa Lango-Bahari la Hormuz liko wazi kwa Kenya pamoja na mataifa mengine rafiki.
-
Jeshi la Iran laonya litatoa jibu kali iwapo mzingiro haramu wa baharini wa Marekani utaendelea
Apr 26, 2026 11:27Kamandi Kuu ya Jeshi la Iran imeonya kuwa kuendelea kwa “uharamia, mzingiro, na uhalifu wa baharini” unaofanywa na vikosi vya Marekani katika eneo, utakabiliwa na jibu kutoka kwa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran yamkamata jasusi mkongwe wa Mossad na magaidi katika operesheni za kitaifa
Apr 26, 2026 11:19Wizara ya Usalama wa Taifa Iran imetangaza kukamatwa kwa jasusi “mzoefu” aliyekuwa akifanya kazi kwa niaba ya utawala wa Kizayuni wa Israel, pamoja na wanachama 15 wa makundi ya kigaidi ya makundi ya wanaotaka kujitenga, kufuatia operesheni zilizofanyika katika mikoa mbalimbali nchini
-
Rais Pezeshkian: Iran haitaingia katika mazungumzo chini ya mashinikizo, vitisho na mzingiro
Apr 26, 2026 09:34Rais Masoud Pezeshkian amekosoa utata na mgongano unaoshuhudiwa kati ya mbinu za mashinikizo zinazotumiwa na Marekani dhidi ya Iran na kile kinachotajwa kuwa ni nia yake ya kushiriki katika mchakato wa kidiplomasia na Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran asema: Tabas itakaririwa katika Ghuba ya Uajemi/ atoa indhari kuhusu kushindwa Marekani
Apr 25, 2026 11:47Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran ametahadharisha kuwa Washington haina uwezo wa kuweka mzingiro wa kijeshi wa majini dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, na kuapa kuwa kushindwa kihistoria wanajeshi wa Marekani huko Tabas na Isfahan kutarudiwa katika maji ya Ghuba ya Uajemi.
-
Waziri wa Michezo wa Italia akataa pendekezo la kuchukua nafasi ya Iran kwenye Kombe la Dunia la FIFA
Apr 25, 2026 09:39Waziri wa michezo wa Italia, Andrea Abodi, amesema kuwa pendekezo la nchi yake kuchukua nafasi ya Iran kwenye Kombe la Soka la Dunia “si sahihi,” na akapinga wazo lolote kuwa timu ya taifa ya nchi hiyo maarufu kama Azzurri itapewa nafasi ya dharura katika mashindano ya ya soka ya FIFA mwaka huu.
-
Saudi Arabia yatarajia kuwapokea kwa ukarimu Wairani wanaoshiriki ibada Hija
Apr 25, 2026 09:34Saudi Arabia imetangaza kuwa imejiandaa kikamilifu kwa msimu wa Hija na inasubiri kwa shauku kuwasili kwa waumini wa Iran wanaoshiriki katika ibada ya Hija Iran, baada ya kufanya maandalizi yote muhimu ili kuhakikisha wanatekeleza ibada zao kwa usalama na faraja.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akutana na viongozi wa Pakistan jijini Islamabad
Apr 25, 2026 09:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Abbas Araqchi, amefika katika mji wa Islamabad, Pakistan na kufanya mazungumzo na viongozi wa ngazi za juu nchini humo.
-
Kiongozi Muadhamu: Umoja wa Wairani umetoa pigo kubwa kwa safu za adui
Apr 25, 2026 06:03Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, amepongeza athari kubwa ya umoja wa kitaifa, akisema mshikamano wa wananchi wa Iran umevuruga kwa kiasi kikubwa safu za maadui.