-
Viongozi wa Iran wamwambia Trump: Hatuna watu wenye msimamo mkali na wenye msimamo wa wastani; sote ni Wairani na wanamapinduzi
Apr 25, 2026 05:53Wakuu wa Mihimili Mitatu ya Iran wamejibu madai ya uongo ya Rais Donald Trump Marekani kwamba kuna mgawanyiko ndani ya nchi na kusema: Hatuna watu wenye msimamo mkali na wenye msimamo wa wastani; sote ni Wairani na wanamapinduzi.
-
Utafiti wa IRIB: Wairani wengi wanaunga mkono msimamo wa mapambano dhidi ya Marekani na Israel
Apr 25, 2026 04:34Baada ya vita vya siku 40 vya muungano wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Iran, utafiti wa kitaifa uliofanywa na Kituo cha Utafiti cha Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB) umeonyesha kuendelea kusimama kidete kwa wananchi katika kuunga mkono vikosi vya ulinzi, mshikamano wa kitaifa na azma madhubuti ya kulinda uwezo wa nchi wa makombora na miundombinu ya kiulinzi.
-
Iran yaonya kuhusu mgogoro wa chakula duniani kutokana na vita vya kigaidi vya Marekani
Apr 25, 2026 04:25Waziri wa Kilimo wa Iran, Gholamreza Nouri, amesema kuwa mashambulizi na vitendo vya uchokozi vya Marekani vina madhara makubwa kwa usalama wa chakula duniani, na vinatoa kikwazo kikubwa katika kufanikisha lengo la “kutokomeza njaa.”
-
Vipi IRGC Imefikia Kuwa na Nguvu na Uwezo Unaoshuhudiwa Hivi Sasa?
Apr 23, 2026 19:05Maadhimisho ya mwaka huu ya kutimia miaka 48 ya kuasisiwa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC yametoa mguso zaidi katika duru za kisiasa na za vyombo vya habari kuliko ilivyowahi kushuhudiwa katika maadhimisho ya miaka iliyopita.
-
Jeshi la Iran la IRGC lasema litazindua zana za kivita zitakazomshangaza adui
Apr 23, 2026 10:59Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema kuwa liko tayari kutangaza mafanikio mapya pamoja na zana za kushangaza za kivita zinazozidi upeo wa kuelewa wa adui, likionya kuwa kila kitendo kipya cha uchokozi kitapata majibu makali.
-
Iran Yalalamikia Matumizi Mabaya ya Ardhi na Anga ya Nchi 5 na Marekani
Apr 23, 2026 10:56Amir Saeed Iravani, balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa, katika barua aliyomwandikia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama, ametoa malalamiko makali kuhusu matumizi mabaya ya Marekani ya ardhi na anga ya nchi tano za eneo katika hujuma za kijeshi dhidi ya Iran. Nchi hizo ambazo zimeafiki ardhi zao kutumiwa kuishambulia Iran ni pamoja na Qatar, Kuwait, Bahrain, Falme za Kiarabu (UAE) na Saudi Arabia.
-
Araghchi: Mzingiro wa bandari za Iran ni uvunjaji wa makubaliano ya usitishaji vita
Apr 23, 2026 10:54Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, ametoa tamko kufuatia shambulio la Marekani dhidi ya meli ya kibiashara ya Iran katika Bahari ya Oman, akisema kwamba kuweka mzingiro dhidi ya bandari za Iran ni uvunjaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Baqaei: Iran Iko tayari kujilinda mkabala wa vitisho vya adui
Apr 23, 2026 09:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza utayari wa Tehran kujilinda dhidi ya mashambulizi na vitisho vya aina yoyote vya adui.
-
Araqchi: Mashambulizi dhidi ya Iran ni chanzo cha ukosefu wa usalama katika Ghuba ya Uajemi
Apr 23, 2026 09:35Mwakilishi Maalumu wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Korea Kusini, ambaye aliwasili Tehran kwa ajili ya mashauriano na viongozi wa Iran, amekutana na kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran.
-
Kiongozi Muadhamu awashukuru Maulamaa wa Kisunni wa Hormozgan
Apr 21, 2026 09:19Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Hosseini Khamenei, ameelezea shukrani zake za dhati kwa wanazuoni na maulamaa wa Kisunni katika mkoa wa kusini mwa Iran wa Hormozgan, akisifu mshikamano wao na tamko lao la kutoa Bay’a yaani kiapo cha utii.