-
Iran yathibitisha kupokea mapendekezo ya wapatanishi yanayolenga kupunguza mvutano
Jul 21, 2026 03:32Iran imethibitisha kupokea mapendekezo na maoni mbalimbali kutoka kwa wapatanishi kadhaa yanayolenga kupunguza mivutano na Marekani, huku Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Esmaeil Baqaei, akisema kuwa Tehran inaendelea na juhudi za kidiplomasia sambamba na hatua zinazochukuliwa na vikosi vya ulinzi vya Iran.
-
Baqaei: Marekani imeonyesha tena sera yake ya uharibifu kwa kushambulia miundombinu ya Iran
Jul 20, 2026 11:20Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amesema kuwa Marekani imeonyesha kwa mara nyingine tena sera yake ya uharibifu baada ya kufanya mashambulizi dhidi ya miundombinu ya Iran.
-
Kusimamishwa Ahadi za Mkataba wa Islamabad: Majibu ya Iran dhidi ya Ukiukaji wa Marekani
Jul 20, 2026 08:05Iran imesimamisha utekelezaji wa ahadi zake chini ya Mkataba wa Islamabad. Akifafanua suala hilo, Kazem Gharibabadi, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, amesema kuwa baada ya Marekani kukiuka wajibu wake chini ya Mkataba wa Maelewano wa Islamabad, Tehran imesimamisha utekelezaji wa ahadi zake zote na kwamba sasa imejikita katika mipango ya kulinda nchi kwa uthabiti mkabala wa hujuma za adui.
-
Spika wa Bunge la Iran: Wito wa Kiongozi wa "Umoja wa Kitaifa" ni muhimu kwa ushindi
Jul 19, 2026 12:51Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge la Iran) Mohammad Baqer Qalibaf amesisitiza kuwa kuzingatia maaagizo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kuhusu kudumisha umoja wa kitaifa ni muhimu kwa ajili ya ushindi katika mapambano dhidi ya adui.
-
Jeshi la Iran lafanya mashambulizi mapya ya droni katika kambi za Marekani huko Kuwait/IRGC yatungua droni ya MQ-9 huko Ahvaz
Jul 19, 2026 12:47Jeshi la Iran lafanya mashambulizi mapya ya droni katika kambi za Marekani huko Kuwait/IRGC yatungua droni ya MQ-9 huko Ahvaz
-
Ayatullah Khamenei awapongeza Wairaqi kwa mahudhurio makubwa katika mazishi ya Kiongozi shahidi
Jul 19, 2026 09:29Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amewashukuru watu wa Iraq kwa mapokezi "makubwa" na mahudhurio yao ya kustaajabisha katika mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, akisema tukio hilo linaonyesha uhusiano mkubwa wa kidini na kihistoria kati ya mataifa ya Iran na Iraq.
-
Ukiukaji wa MoU wa Marekani unathibitisha saini ya rais wa Marekani 'haina thamani'
Jul 19, 2026 03:44Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema ukiukaji wa mara kwa mara wa Marekani wa Mkataba wa Maelewano wa Islamabad (MoU) umethibitisha tena kwamba sahihi ya rais wa Marekani "haina thamani kabisa na ni batili."
-
Marekani yakiri wanajeshi wake wameuawa katika shambulizi la Iran nchini Jordan
Jul 19, 2026 03:29Jeshi la Marekani limethibitisha kwamba wanajeshi wake wasiopungua wawili wameuawa katika mashambulizi ya Iran yaliyolenga mali na kambi za kijeshi za za Marekani nchini Jordan.
-
Iravani: Kutochukua hatua UN kunahalalisha haki ya Iran ya kujibu mashambulizi
Jul 19, 2026 03:20Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa, Amir Saeid Iravani, ameliandikia barua Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Katibu Mkuu wa umoja huo kufuatia uchokozi wa Marekani dhidi ya Iran, kushambuliwa miundombinu na mauaji ya raia wa Iran.
-
Op. Nasr-2: IRGC yaharibu rada ya kijeshi ya Marekani huko Kuwait katika shambulio la kulipiza kisasi
Jul 18, 2026 11:13Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeharibu kituo cha rada cha jeshi la Marekani katika Kituo cha Anga cha Ali Al Salem na kushambulia mkusanyiko wa wanajeshi wa nchi hiyo katika Kambi ya Arifjan huko Kuwait katika wimbi la 18 la Operesheni Nasr 2.