-
Iran: Dunia imechoshwa na hadithi za uongo za Marekani na Israel
Mar 23, 2026 05:30Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, ameashiria msimamo wa Katibu Mkuu wa Muungano wa Kijeshi wa Nchi za Magharibi-NATO- kuhusu kukataa madai ya hivi karibuni ya maafisa wa utawala wa Kizayuni Israel kuhusu tishio la makombora ya Iran kwa Ulaya na kuandika katika mtandao wa X kuwa dunia imechoka na simulizi za uongo za Marekani na Israel.
-
Taarifa ya Ayatullah Hajj Sheikh Muhammad Jawad Fadhil Lankarani, Kuhusu Hatua Isiyofaa ya Al-Azhar
Mar 23, 2026 04:44Katika kujibu hatua ya hivi karibuni ya viongozi wa Al-Azhar, Chuo Kikuu cha Kidini cha nchini Misri ya kulaani hatua ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kulipiza kisasi dhidi ya vituo vya kijeshi vya Marekani katika ardhi za nchi za Kiarabu za Ghuba ya Ujemi, viongozi tofauti wa kidini akiwemo Ayatullah Sheikh Muhammad Jawad Fadhil Lankarani, wametoa taarifa wakikosoa vikali hatua hiyo ya kibaguzi ya wanazuoni wa Al- Azhar.
-
Mwisho wa makubaliano ya Atlantiki; kwa nini Marekani imetengwa katika vita vyake vya kichokozi dhidi ya Iran?
Mar 22, 2026 07:30Duru ya pili ya hujuma za kijeshi za Marekani na utawala wa Kizayuni imekuwa nukta muhimu katika historia ya mikataba na makubaliano ya kijeshi katika ulimwengu wa Magharibi.
-
Jeshi la Iran latungua ndege nyingine ya kivita aina ya F15 ya adui mvamizi, Sepah inaendelea kutoa dozi
Mar 22, 2026 07:14Jeshi la Iran limetangaza kuwa limetungua ndege ya kivita aina ya F15 ya maadui wavamizi, Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, kusini mwa nchi.
-
Kamanda Mousavi: Iran sasa inadhibiti kikamilifu anga ya Israel
Mar 22, 2026 06:14Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ametangaza kuwa makombora ya Iran sasa yanadhibiti kikamilifu anga ya utawala ghasibu wa Israel.
-
Jeshi la Iran limelenga Uwanja wa Ndege wa Ben‑Gurion kwa droni
Mar 22, 2026 05:04Msemaji wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa jeshi hilo limetekeleza shambulio kwa mafanikio dhidi ya Uwanja wa Ndege wa Ben‑Gurion katika mji wa Lod umbali wa kilomita 15 kusini mashariki mwa Tel Aviv, kwa kutumia droni ya kisasa ya Arash‑2.
-
Iran yatoa onyo kuhusu hujuma dhidi miundombinu ya nishati na mafuta
Mar 22, 2026 05:03Msemaji wa Kamandi ya Jeshi la Iran ya Khatam al-Anbiyaa (SAW) ametoa onyo kali kuhusu uwezekano wa kushambuliwa kijeshi miundombinu ya nishati na mafuta ya Iran.
-
Qalibaf: Anga ya Israel imekuwa "shamba la bibi", ni wakati wa kutekeleza mpango unaofuata
Mar 22, 2026 03:50Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema inaonekana kuwa umewadia wakati wa kutekeleza mpango unaofuata uliopangwa hapo awali kwa ajili ya mashambulizi zaidi dhidi ya Israel.
-
The Independent: Trump analazimika kuipa Iran inachokitaka ili kujinasua kwenye maangamizi
Mar 22, 2026 03:49Gazeti la Uingereza la Independent limeandika kuwa, Rais Donald Trump wa Marekani amenasa katika maangamizi kwa kuanzisha vita dhidi ya Iran na analazimika kuipatia Iran inachokitaka ili kukomesha vita hivyo.
-
Mauaji ya kigaidi ya Marekani na Israel dhidi ya viongozi wa Iran na mmomonyoko wa sheria za kimataifa
Mar 21, 2026 07:04Mauaji ya kigaidi dhidi ya Ali Larijani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran mnamo Machi 17, 2026, siku 18 tu baada ya mauaji mengine ya kigaidi dhidi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Seyyed Ali Khamenei, ni zaidi ya suala la kuongezeka tu mashambulizi ya kijeshi. Yanaangazia wazi upuuzaji wa sheria za kimataifa zilizobuniwa baada ya Vita vya Pili vya Dunia 1945.