-
Iran, US zakamilisha duru ya pili ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana ya nyuklia, Geneva
Feb 17, 2026 10:09Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, duru ya pili ya mazungumzo ya nyuklia yasiyo ya ana kwa ana kati ya Iran na Marekani imemalizika mjini Geneva, Uswisi.
-
Kiongozi Muadhamu amjibu Trump na kusema, Meli za kivita zinaweza kuzamishwa baharini
Feb 17, 2026 09:17Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amejibu vitisho vya mara kwa mara vya kijeshi kutoka Marekani dhidi ya Iran, akisema kuwa silaha zenye uwezo wa kuzamisha manowari za Marekani ni “hatari zaidi” kuliko meli hizo za kivita zenyewe.
-
Somalia kuanza kutoa pasipoti za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)
Feb 17, 2026 07:51Somalia inatarajiwa kuanza kutoa hati ya kusafiria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwa raia wake; ikiungana na nchi nyingine wanachama katika kutumia hati ya kusafiria ya kikanda.
-
Iran yaadhimisha Siku ya Arobaini ya Mashahidi wa ghasia za kigaidi
Feb 17, 2026 07:12Wairani leo wanashiriki katika hafla kubwa ya kitaifa mjini Tehran kuadhimisha siku ya arobaini tangu kuuawa kishahidi kwa watu waliopoteza maisha yao katika mashambulizi ya kigaidi ya Januari 8 na 9.
-
Idadi ya vifo vya Kimbunga Gezani yapanda hadi 59 nchini Madagascar
Feb 17, 2026 07:11Idadi ya watu waliopoteza maisha kufuatia Kimbunga Gezani nchini Madagascar imeongezeka hadi 59, huku watu 804 wakijeruhiwa. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya hivi karibuni iliyotolewa na Ofisi ya Kitaifa ya Usimamizi wa Hatari na Maafa (BNGRC).
-
Mtaalamu: Sera ya biashara ya Marekani barani Afrika inaendeshwa kwa mabavu na ghiliba za kisiasa
Feb 17, 2026 07:10Marekani inajaribu kudumisha nafasi yake barani Afrika kupitia matumizi ya mabavu na ghiliba za kisiasa, huku ikizingatia zaidi nishati na madini muhimu, tofauti na ushirikiano mpana wa kiuchumi wa China katika bara hilo.
-
UN yatoa wito mpya wa kutokomeza ukoloni
Feb 17, 2026 07:09Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amesema ingawa zaidi ya mataifa 100 yamepata uhuru tangu mwaka 1945, mchakato wa kuondoa ukoloni bado haujakamilika. Ametoa kauli hiyo akifungua kikao cha mwaka 2026 cha Kamati Maalum ya Umoja wa Mataifa kuhusu Kutokomeza Ukoloni,
-
Viongozi wa Afrika watangaza mshikamano na watu wa Palestina
Feb 17, 2026 04:16Viongozi wa nchi za Afrika wametangaza mshikamano wao na watu wa Palestina na haki yao ya kujitawala.
-
Iran: Ulimwengu unawajibika kukabiliana na ukiukaji wa haki za binadamu wa Israel
Feb 17, 2026 03:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa jamii ya kimataifa inawajibika kukabiliana na hatua za utawala wa Israel za kuendelea kukiuka pakubwa sheria katika eneo la Asia Magharibi.
-
Niger na Algeria zatangaza kuanza 'mchakato mpya' baada ya mazungumzo ya ujenzi wa bomba jipya la gesi mjini Algiers
Feb 17, 2026 03:44Rais wa Niger ametangaza kuanza kwa "mchakato mpya" kati ya nchi hiyo na Algeria.