-
Wakuu wa zamani wa usalama wamwambia Netanyahu: Komesha ugaidi wa Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi
Jun 18, 2026 11:28Mawaziri wakuu wawili wa zamani wa Israel, pamoja na watu mashuhuri kutoka Israel na Marekani, wakuu wa zamani wa mashirika ya usalama, na maafisa kadhaa wa zamani katika taasisi mbalimbali za usalama, wamesaini barua iliyoelekezwa kwa Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu jana Jumatano, wakiitaka serikali na mashirika yake kuchukua hatua za haraka za kukabiliana na kile walichokiita "ugaidi wa Kiyahudi" katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu huko Palestina.
-
Milio ya risasi yasikika katika mji mkuu wa Niger, Niamey
Jun 18, 2026 10:06Milio ya risasi imesikika mapema leo Alkhamisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Diori Hamani mjini Niamey, nchini Niger, miezi kadhaa baada ya shambulio kubwa la waasi katika eneo hilo hilo.
-
Je, vita vya Iran vilisambaratisha vipi ngano ya nguvu isiyoshindwa ya Marekani?
Jun 18, 2026 08:22"Vita na Iran vimefichua ukweli mchungu kwa Marekani; Trump alifanya makosa makubwa na hatari kwa kuanzisha vita hivi na hatimaye kutoka kwenye vita akiwa dhaifu kijeshi, kidiplomasia na kiuchumi."
-
Rais Pezeshkian: Taifa la Iran limejifunza kutokubali kudhalilishwa kutoka kwa Kiongozi aliyeuawa shahidi
Jun 18, 2026 06:01Rais Masoud Pezeshkian amesema taifa la Iran limejifunza kutokubali kudhalilishwa kutoka kwa Kiongozi aliyeuawa shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.
-
Shirika la Anga za Juu la Iran kuzindua satalaiti ya Pars-2
Jun 18, 2026 05:58Shirika la Masuala ya Anga za Juu la Iran linasonga mbele kwa kasi mpya, huku Waziri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano akitangaza mipango ya uzinduzi ujao wa satalaiti ya "Pars 2" na kupelekwa angani Shahid Soleimani Satellite Constellation ifikapo mwisho wa mwaka huu.
-
Hamas: Kamwe hatutakabidhi silaha zetu kwa Israel na Marekani
Jun 18, 2026 05:57Naibu mkuu wa Idara ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) nje ya nchi ametangaza kwamba harakati hiyo kamwe haitakabidhi silaha zake kwa Israel na Marekani.
-
Marais wa Iran na Marekani watia saini kidijitali Makubaliano ya kumaliza vita
Jun 18, 2026 04:27Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani sasa imetiwa saini rasmi na marais wa nchi hizo mbili baada ya maandishi yake kukamilishwa, na hivyo makubaliano hayo kuanza kutekelezwa. Hayo yametangazwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Jumatano usiku.
-
"Bila Israel, kusingekuwa na Marekani"; Balozi wa Washington huko Tel Aviv aibua hasira za Wamarekani
Jun 18, 2026 04:25Matamshi ya balozi wa Marekani huko Israel, Mike Huckabee, yamezua wimbi la hasira na ukosoaji mkubwa katika duru za kisiasa na vyombo vya habari vya Marekani, baada ya kusema kwamba Marekani "haingekuwepo bila Israel," katika taarifa iliyozusha mjadala mkubwa kuhusu ushawishi wa Israel ndani ya duru za kufanya maamuzi za Marekani na mipaka ya majukumu ya balozi wa Marekani huko Tel Aviv.
-
Kwa nini umoja wa nyanja ni muhimu kwa Iran na kusambaratika kwake ni muhimu kwa Israel?
Jun 17, 2026 12:18Wakati Iran na Marekani zilipokuwa zinakaribia kufikia mapatano ya awali kuhusu kusimamisha vita, utawala wa Kizayuni kwa mara nyingine tena siku ya Jumapili (Juni 14, 2026) ulishambulia viunga vya mji wa Beirut, na hivyo kuendelea kukiuka usitishavi vita.
-
Jeshi la Iran laionya Israel kuhusu ukiukaji usitishaji vita Lebanon
Jun 17, 2026 12:10Kamandi Kuu ya Majeshi ya Iran, Khatam al-Anbiya imeuonya utawala wa Israel na kuutaka usitishe mara moja ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliiano ya usitishaji vita kusini mwa Lebanon, au ukabiliwe na “jibu kali” la majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.