May 07, 2024 06:38
Huku kukiwa na ripoti kwamba Wapalestina 100,00 wameamriwa kuhama Rafah kusini mwa Ukanda wa Ghaza kabla ya uvamizi wa kijeshi uliopangwa kufanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel, mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayotoa huduma za kibinadamu yamesisitiza kuwa hayana nia ya kuondoka katika mji huo muhimu zaidi kwa mahitaji ya misaada ya kibinadamu.