Kamanda Mwandamizi: Israel imeshindwa na Muqawama Ghaza, viongozi watamatishe vita
Yitzhak Barik, Jenerali mstaafu wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kuwa jeshi la utawala huo haramu limeshindwa na Muqawama wa Palestina katika vita vya Ukanda wa Ghaza na kutaka viongozi wa utawala huo watangaze utamatishaji wa vita hivyo.
Baada ya kupita zaidi ya miezi sita tangu utawala wa Kizayuni wa Israel uivamie Ghaza bila ya kupata matunda wala mafanikio yoyote, utawala huo unazidi kuzama kwenye kinamasi cha migogoro yake ya ndani na nje siku baada ya siku.
Katika muda wote huu, utawala katili wa Kizayuni haujapata mafanikio mengine isipokuwa ya kufanya jinai, mauaji, uharibifu, uhalifu wa kivita, kukiuka sheria za kimataifa, kushambulia mashirika ya utoaji misaada na kulinakamisha kwa njaa eneo la Ghaza.