-
Hamas: Msikiti wa al Aqsa ni mstari mwekundu kwa taifa la Palestina na Waislamu
Jul 18, 2020 03:35Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, mji mtakatifu wa Quds pamoja na Msikiti wa al Aqsa ambao ni Kibla cha Kwanza cha Waislamu, ni mstari mwekundu kwa taifa la Palestina na kambi ya muqawama na kwamba kuyaunga mkono maeneo hayo matakatifu ni jukumu la kidini na kimaadili la mataifa yote ya Waislamu.
-
Mshauri wa Abbas: Chokochoko mpya za Israel zitaibua Intifadha ya 3 ya Palestina
Jul 05, 2020 22:56Mshauri wa Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina ameonya kuwa, Intifadha ya Tatu ya wananchi wa Palestina inanukia na bila shaka itaibuka mara moja iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utatekeleza mpango wake wa kulipora na kuliunganisha eneo la Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan na ardhi za Palestina zilizopewa jina la Israel.
-
Intifadha, njia pekee ya kukabiliana na mpango wa kulitwaa eneo la Ukingo wa Magharibi
Jun 28, 2020 23:25Mkuu wa Kamati ya Kuunga mkono Mapinduzi ya Wananchi wa Palestina amesema kuwa mapambano ya Intifadha ndio njia pekee ya kukabiliana na mpango wa utawala wa kizayuni wa Israel wa kutaka kulitwaa eneo la Ukingo wa Magharibi.
-
Wazayuni wauhujumu Msikiti wa Al Aqsa
Jun 10, 2020 00:24Makumi ya walowezi wa Kizayuni, wakiwa wanapata himaya ya wanajeshi wa utawala wa Israel wameuhujumu Msikiti wa Al Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem).
-
Mufti wa Palestina atoa wito kwa Waislamu kuunga mkono malengo ya Palestina
May 31, 2020 23:20Mufti wa Palestina ameutaka Umma wa Kiislamu na Kiarabu kutekeleza majukumu yao kuhusu Quds na Palestina na kuyatetea matukufu yake.
-
HAMAS yalaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Kibla cha Kwanza cha Waislamu
May 30, 2020 07:55Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, harakati hiyo kamwe haitoruhusu utawala wa Kizayuni uendelee kufanya jinai dhidi ya Msikiti wa al Aqsa (Kibla cha Kwanza cha Waislamu).
-
Askari wa Kizayuni washambulia Wapalestina katika Swala ya Idi
May 24, 2020 03:27Wanjeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewashambulia Wapalestina waliokuwa wamefika katika Msikiti wa Al-Aqsa mjini Quds kwa ajili ya ibada.
-
Hotuba ya Kiongozi Muadhamu kwa mnasaba na Siku ya Kimataifa ya Quds
May 23, 2020 06:00Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu leo (Ijumaa) katika hotuba yake kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Quds amezungumzia suala la kuanza awamu mpya ya mapambano ya Palestina baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kudhihiri mrengo wa muqawama sambamba kubadilika mlingano wa nguvu kwa maslahi ya wanamapambano na ametoa miongozo saba muhimu kuhusu jinsi ya kuendeleza Jihadi kubwa na takatifu ya sasa.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kuhusu kukaribia kuangamia utawala wa Kizayuni katika eneo
May 22, 2020 22:08"Bila shaka kirusi cha Uzayuni hakitadumu kwa muda mrefu na kwa kutegemea hima, imani, ghera ya vijana, mizizi ya kirusi hicho itang'olewa na kuondolewa katika eneo".
-
Chama cha Republican cha Tunisia: Umoja na muqawama, njia pekee ya kuikomboa Palestina
May 22, 2020 03:37Katibu Mkuu wa chama cha Republican cha Tunisia amesema utawala ghasibu wa Israel hauelewi lugha nyingine isipokuwa ya mapambano na kusisitiza kuwa, "umoja na muqawama ndiyo njia pekee ya kuikomboa Palestina."