Watu 45 wafariki dunia katika ajali ya basi la wafanyaziara wa Pasaka nchini Afrika Kusini
Watu wasiopungua 45 wamefariki dunia nchini Afrika Kusini wakati basi lililokuwa limebeba wafanyaziara wa Pasaka lilipotumbukia kwenye daraja jana Alhamisi.
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametuma salamu za rambirambi kwa Botswana na kuahidi msaada kwa nchi hiyo. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi yake.
Serikali ya mkoa imesema miili mingi iliungua moto kiasi cha kutotambulika na kubaki ndani ya basi hilo.
Waziri wa Uchukuzi wa Afrika Kusini Sindisiwe Chikunga amesema uchunguzi kuhusu ajali hiyo unaendelea na akatoa rambirambi zake kwa familia za waliofariki.
Kwa mujibu wa mashirika ya habari, Kanisa la Kikristo la Kizayuni lina makao yake makuu mjini Moria na ziara zake za Pasaka huvutia mamia ya maelfu ya watu kutoka kote Afrika Kusini na nchi jirani pia.
Huu ni mwaka wa kwanza wa safari ya Pasaka kuelekea Moria kufanyika tangu lilipozuka janga la Covid-19.../