Mivutano ya kisiasa yaongezeka kati ya Sudan na Sudan Kusini
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i15787-mivutano_ya_kisiasa_yaongezeka_kati_ya_sudan_na_sudan_kusini
Duru za nchini Sudan zimekosoa upuuzaji unaofanywa na Sudan Kusini katika kuwadhibiti waasi waliopo katika maeneo ya mipaka ya nchi mbili hizo.
(last modified 2026-02-25T03:34:48+00:00 )
Sep 21, 2016 10:31 UTC
  • Mivutano ya kisiasa yaongezeka kati ya Sudan na Sudan Kusini

Duru za nchini Sudan zimekosoa upuuzaji unaofanywa na Sudan Kusini katika kuwadhibiti waasi waliopo katika maeneo ya mipaka ya nchi mbili hizo.

Afisa mmoja wa ngazi ya juu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan ambaye hakutajwa jina lake litajwe ametishia kuwa Sudan Kusini inapasa kuchukua hatua za lazima na kuyafukuza makundi ya uasi yaliyoko katika maeneo ya mpakani ya nchi hiyo.  Afisa huyo wa Sudan amesema kuwa nchi hiyo itafunga mipaka yake na jirani yake  Sudan Kusini iwapo haitatekeleza ahadi yake ya kuyafukuza makundi ya uasi yanayopigana na Khartoum.

Hii ni katika hali ambayo Taban Deng Makamu wa Rais wa Sudan Kusini  wiki kadhaa zilizopita alifanya safari huko Khartoum mji mkuu wa Sudan kwa ajili ya mashauriano ya kisiasa na viongozi wa ngazi za juu wa nchi hiyo; ambapo ajenda kuu ya mazungumzo yao ya kisiasa ilikuwa ni  kuipatia ufumbuzi mivutano ya kisiasa kati ya nchi mbili hizo.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan akiwa na Taban Deng Makamu wa Rais wa Sudan Kusini (kulia) ziarani mjini Khartoum hivi karibuni

Baada ya mazungumzo hayo Deng aliwahakikishia viongozi wa Khartoum kuwa waasi walipo katika maeneo ya mpakani watafurushwa huko Sudan Kusini katika muda wa siku 21. Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan Kusini pia siku kadhaa zilizopita ilisisitiza kuhusu kupatiwa haraka iwezekakanavyo ufumbuzi mivutano ya kisiasa iliyopo.