Ufaransa kushirikiana na nchi za Afrika katika mapambano dhidi ya ugaidi
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i19993-ufaransa_kushirikiana_na_nchi_za_afrika_katika_mapambano_dhidi_ya_ugaidi
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa Bernard Cazeneuve amesema nchi yake itapanua ushirikiano wake na bara la Afrika katika kupambana na ugaidi.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Nov 23, 2016 00:48 UTC
  • Ufaransa kushirikiana na nchi za Afrika katika mapambano dhidi ya ugaidi

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa Bernard Cazeneuve amesema nchi yake itapanua ushirikiano wake na bara la Afrika katika kupambana na ugaidi.

Cazeneuve ameyasema hayo katika kikao cha pamoja na mawaziri wa mambo ya ndani wa nchi 11 za Kiafrika kilichofanyika mjini Paris na kusisitiza kwamba mapambano dhidi ya ugaidi kwa lengo la kugundua na kuzuia vitendo vya kufurutu mpaka yataendelea kwa msukumo mkubwa zaidi.

Mawaziri wa mambo ya ndani wa nchi za Afrika ikiwemo Benin, Cameroon, Ivory Coast, Guinea, Mali, Mauritania, Niger, Senegal, Chad na Togo walikutana na mwenzao wa Ufaransa jana Jumanne  mjini Paris kujadili na kubadilishana mawazo kuhusu njia za kupambana na ugaidi na misimamo ya kufurutu mpaka.

Boko Haram ni moja ya makundi ya kigaidi yanayohatarisha usalama katika nchi za magharibi mwa Afrika

Katika kikao chao hicho mawaziri hao walikubaliana juu ya utoaji mafunzo kwa askari polisi kwa ajili ya kupambana na misimamo ya kufurutu mpaka hasa miongoni mwa vijana na kuongeza operesheni za mazoezi ya kupambana na ugaidi.../