Maelfu ya raia wa CAR wakimbilia mkoa wa Equator Kongo DR
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i30554-maelfu_ya_raia_wa_car_wakimbilia_mkoa_wa_equator_kongo_dr
Habari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zinaarifu kuwa, tangu mwezi Mei mwaka huu, hadi hivi sasa zaidi ya wakimbizi elfu 30 kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati, wameingia katika mkoa wa Equator wa kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jun 16, 2017 10:56 UTC
  • Maelfu ya raia wa CAR wakimbilia mkoa wa Equator Kongo DR

Habari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zinaarifu kuwa, tangu mwezi Mei mwaka huu, hadi hivi sasa zaidi ya wakimbizi elfu 30 kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati, wameingia katika mkoa wa Equator wa kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) imesema kuwa, hadi sasa maelfu ya wakimbizi kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati wapo katika mkoa huo. Shirika hilo limeongeza kuwa, raia hao wa CAR wamelazimika kuyakimbia makazi yao kwenda ughaibuni kutokana na mashambulizi ya makundi ya Anti-Balaka na Seleka ambayo yamekuwa yakiendesha hujuma za ulipizaji kisasi kati yao.

Jamii ya Waislamu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wanaokabiliwa na mauaji ya magaidi wa Kikristo

Hii ni katika hali ambayo, licha ya Umoja wa Mataifa kuahidi kutoa misaada kwa ajili ya wakimbizi hao, lakini hadi sasa bado wanaishi katika mazingira magumu kutokana na kukosa misaada hiyo. Jamhuri ya Afrika ya Kati ilitumbukia katika mchafuko mwaka 2013, baada ya waasi wa Seleka kumpindua aliyekuwa rais wa nchi hiyo, François Bozizé. Baada ya tukio hilo kundi la Kikristo lenye misimamo ya kuchupa mipaka la Anti-Balaka lilianzisha mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wasio na hatia na kuua maelfu ya watu wa jamii hiyo.

Magaidi wa Kikristo wa Anti-Balaka

Hayo yanajiri katika hali ambayo, Jamhuri ya Afrika ya Kati kuna maelfu ya askari wa Umoja wa Mataifa wanaosimamia amani.