-
Niger yasimamisha vyombo tisa vya habari vya Ufaransa
May 10, 2026 09:28Serikali ya Niger imetangaza kusimamisha shughuli za vyombo tisa vya habari vya Ufaransa, ikieleza kuwa hatua hiyo imechukuliwa kutokana na “usambazaji wa mara kwa mara wa maudhui yanayoweza kuhatarisha kwa kiasi kikubwa utulivu wa umma, umoja wa taifa, mshikamano wa kijamii, na uthabiti wa taasisi za Jamhuri.”
-
Watu 70 wauawa kaskazini mashariki mwa Kongo; Umoja wa Mataifa walaani ghasia
May 10, 2026 07:37Kwa uchache watu 70, wengi wao wakiwa raia, wameuawa katika shambulio lililofanywa na watu wenye silaha waliohusishwa na wanamgambo wa CODECO, kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Wapinzani Afrika Kusini waapa kumuondoa madarakani Ramaphosa
May 09, 2026 09:54Julius Malema, kiongozi wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF) nchini Afrika Kusini, amemtaka Rais Cyril Ramaphosa wa nchi hiyo ajiuzulu haraka iwezekanavyo na taratibu za kumfungulia mashtaka zianze.
-
Burundi kufanya uchaguzi wa rais Mei 3 mwaka ujao
May 09, 2026 09:47Burundi itafanya uchaguzi wa rais Mei 3 mwaka ujao. Habari hiyo ilitangazwa Ijumaa na Tume ya Uchaguzi, wakati wa mkutano uliosusiwa na upinzani.
-
Rais Tshisekedi asema huenda akagombea muhula wa tatu wa urais, Kongo
May 07, 2026 11:13Rais Félix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amezungumzia uwezekano wa kugombea kiti cha urais kwa muhula wa tatu, akisema atakubali kuendelea kuiongoza nchi hiyo iwapo ataungwa mkono na Wakongo kupitia kura ya maoni.
-
Rais wa Sudan Kusini awafuta kazi Mkuu wa Jeshi na Waziri wa Fedha
May 07, 2026 10:50Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amewafukuza kazi Mkuu wa Jeshi na Waziri wa Fedha. Waziri wa Fedha alikuwa amehudumu katika wadhifa huo chini ya wiki mbili.
-
Boko Haram yauwa wanajeshi 23 katika eneo la Ziwa Chad
May 06, 2026 10:49Takriban wanajeshi 23 wa Chad wameuawa na 26 kujeruhiwa katika shambulio la wanamgambo wa Boko Haram kwenye kituo cha kijeshi katika eneo la Ziwa Chad.
-
Afrika Kusini yabaini maambukizi ya virusi vya Hanter vinavyohusishwa na meli ya utalii
May 06, 2026 10:24Afrika Kusini imebaini virusi kwa jina la Hanter aina ya Andes ambavyo hueneza maambukizi kutoka kwa binadamu kwenda kwa binadamu katika watu wawili waliotoka kwenye meli iliyokumbwa na mlipuko wa ugonjwa huo. Haya yameelezwa leo bungeni na Waziri wa Afya wa nchi hiyo.
-
Marekani yatuhumiwa kulazimisha makubaliano ya afya na mikataba ya madini nchini Zambia
May 06, 2026 08:04Zambia imeishutumu Marekani kwa jaribio la kuhusisha makubaliano ya ufadhili wa sekta ya afya na mikataba ya uchimbaji madini yake ya kimkakati. Hayo yamebainika baada ya balozi wa Marekani anayemaliza muda wake kuikosoa serikali ya Zambia kwa madai ya ufisadi, udhaifu wa utawala, na ukosefu wa ushirikiano na programu za misaada ya Marekani.
-
Sudan yazituhumu Imarati na Ethiopia kushambulia uwanja wa ndege wa Khartoum
May 05, 2026 11:41Sudan leo Jumanne imrudisha nyumbani balozi wake nchini Ethiopia kwa mashauriano na kuzituhutumu Ethiopia na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kuwa zimehusika na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) katika uwanja wa ndege wa Khartoum.