-
Tunisia yajitoa kwenye Mahakama ya Haki za Binadamu na Watu ya Umoja wa Afrika
Mar 23, 2025 23:01Tunisia imetangaza kujitoa katika Mahakama ya Haki za Binadamu na Watu ya Umoja wa Afrika (AfCHPR), jambo linaloashiria kupuuza serikali ya Tunis masuala ya haki na kesi zinazoendeshwa katika nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika.
-
RSF yaua raia 45 Al-Malha; jeshi la Sudan lasonga mbele
Mar 23, 2025 07:25Zaidi ya raia 45 wameuawa katika shambulio la Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) katika eneo la Al-Malha, yapata kilomita 210 kaskazini mwa El Fasher, magharibi mwa Sudan.
-
Baada ya Ikulu, Jeshi la Sudan lateka Benki Kuu na maeneo muhimu ya mji mkuu Khartoum
Mar 23, 2025 03:02Jeshi la Sudan jana Jumamosi liliendeleza ushindi wake kwa kuiteka tena Benki Kuu na maeneo kadhaa ya kimkakati na majengo ya serikali katikati mwa Khartoum, yakiwemo pia makao makuu ya Mkuu wa Ujasusi.
-
Kutimuliwa mfululizo viongozi Tunisia; kunani?!
Mar 23, 2025 03:02Tunisia imeshuhudia mabadiliko ya mfululizo, ya mara kwa mara na ya ghafla katika nafasi ya waziri mkuu tangu Kais Saied aingie madarakani na kushika wadhifa wa urais.
-
Maharamia wa Kisomali waachilia huru meli baada ya siku kadhaa za kuiteka
Mar 23, 2025 03:00Maharamia wa Kisomali wameachilia huru meli iliyokuwa inapeperusha bendera ya Yemen ambayo waliiteka nyara tarehe 16 mwezi huu wa Machi katika pwani ya Somalia.
-
Jeshi la Uganda: Tumeua waasi zaidi ya 200 mashariki ya DRC
Mar 22, 2025 23:17Jeshi la Uganda limetangaza habari ya kuwaua mamia ya wapiganaji wa kundi la waasi wa CODECO baada ya kushambulia kambi ya jeshi la Uganda katika mpaka wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Mamia ya waasi wa Fano wauawa katika operesheni ya jeshi la Ethiopia
Mar 22, 2025 23:10Wanajeshi wa Ethiopia wamewaua zaidi ya wapiganaji 300 wa kundi lenye silaha la Fano, washirika wao wa zamani dhidi ya waasi katika eneo la Tigray, katika siku mbili za mapigano mapya katika eneo la kaskazini la Amhara.
-
Shambulio la kigaidi kwenye msikiti nchini Niger laua makumi ya watu
Mar 22, 2025 03:31Makumi ya watu wameuawa shahidi katika shambulio la kundi la kigaidi la ISIS kwenye msikiti mmoja kusini magharibi mwa Niger.
-
UN: Zaidi ya 100,000 wamekimbilia nchi jirani kutokana na mapigano Congo DR
Mar 22, 2025 03:29Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, zaidi ya watu 100,000 wamekimbilia nchi jirani kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya vikosi vya usalama na kundi la waasi la March 23 (M23) katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
-
Netumbo Nandi aapishwa kuwa Rais wa kwanza mwanamke wa Namibia
Mar 21, 2025 11:12Netumbo Nandi Ndaitwah ameapishwa leo Ijumaa kuwa Rais wa kwanza mwanamke wa Namibia, baada ya kushinda uchaguzi mwaka jana.