-
Umoja wa Mataifa: Hali katika Ukanda wa Gaza ni maafa kikamilifu
Jul 26, 2024 23:03Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, hali katika Ukanda wa Gaza iliyosababishwa na mashambulizi ya Israel ni maafa kamili ambayo hayajawahi kuonekana katika medani yoyote ya vita.
-
HAMAS: Kauli ya Marekani ni uongo mtupu, Wapalestina Ghaza wanauawa kwa silaha zake
Jul 26, 2024 09:29Mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: "Madai ya Washington kwamba inatiwa wasiwasi na hali ya kibinadamu na inasikitishwa na machungu na mateso wanayopata watu wa Ghaza ni uongo wa Kimarekani".
-
Hizbullah yashambulia maeneo kadhaa Israel kwa droni na makombora
Jul 26, 2024 09:16Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imeanzisha mashambulizi makubwa dhidi ya maeneo ya kijeshi ya utawala ghasibu wa Israel, huku kukiwa na hujuma na mashambulio ya Israel kusini mwa Lebanon na mashambulizi yanayoendelea dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Ripoti: Israel inatumia maji kama silaha katika vita vya mauaji ya kimbari Gaza
Jul 26, 2024 04:15Utawala wa Kizayuni wa Israel umekuwa ukitumia maji kama silaha ya vita dhidi ya Wapalestina huko Gaza, ukionyesha kutojali maisha ya binadamu na kukiuka sheria za kimataifa.
-
Iran yakaribisha makubaliano ya kurejeshwa safari za ndege mjini Sana'a, Yemen
Jul 25, 2024 23:48Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekaribisha taarifa ya mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Yemen kuhusiana na makubaliano yaliyofikiwa ya kurejeshwa safari za ndege katika uwanja wa ndege wa Sana'a mji mkuu wa Yemen na kutatuliwa matatizo ya fedha na kibenki kote nchini humo.
-
Russia yawaambia Wazayuni: Hakuna haja ya kuendelea vita Asia Magharibi
Jul 25, 2024 23:45Msemaji wa Ikulu ya Russia amemshambulia vikali waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu, na kusema kuwa, Moscow iko huru katika maamuzi yake na haichukui amri kutoka kwa Wazayuni na inaamini hakuna haja ya kuendelea vita katika eneo la Asia Magharibi.
-
Tuhuma za Netanyahu dhidi ya Iran mbele ya Kongresi ya Marekani na njozi yake kuhusu Baitul Muqaddas
Jul 25, 2024 23:07Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni amehutubia Bunge la Marekani la Kongresi, ambapo mbali na kutoa shukurani kwa uungaji mkono wa kila hali wa serikali ya Marekani kwa duru mpya ya mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala huo katika Ukanda wa Ghaza, kwa mara nyingine ameibua tuhuma dhidi ya Iran na kuzungumzia njozi aliyonayo kuhusu Baitul Muqaddas.
-
Vladimir Putin atahadharisha kuhusu hali mbaya ya Asia Magharibi
Jul 25, 2024 07:50Rais Vladimir Putin wa Russia ametahadharisha kuhusu hali inayozidi kutokota ya eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Onyo la Mashirika ya Kimataifa kuhusu hali mbaya ya wagonjwa huko Gaza
Jul 25, 2024 05:59Wagonjwa katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hatari ya kifo kutokana na kuendelea mashambulizi ya mabomu ya utawala wa Kizayuni na vilevile hatua ya utawala huo ya kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia katika ukanda huo.
-
Amnesty International: Marekani mshirika wa Israel katika mauaji ya kimbari Palestina
Jul 25, 2024 03:41Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International imeonya Marekani kuhusu kuupa silaha utawala wa Kizayuni katika vita vya Gaza na kutangaza kuwa, Washington ni mshirika wa utawala huo katika mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.