Alkhamisi, Mei 26, 2016
Leo ni Alhamisi tarehe 19 Shaaban mwaka 1437 Hijiria, inayosadifiana na tarehe 26 Mei 2016 Miladia
&&&
Siku kama ya leo miaka 135 iliyopita sawa na tarehe 26 Mei mwaka 1881, Ufaransa ilianza rasmi kuikoloni Tunisia. Kabla ya hapo Ufaransa ilianza kupenya Tunisia kupitia harakati za kiuchumi na kibiashara. Aidha kwa miaka kadhaa Tunisia ilikuwa ikidhibitiwa na Ufaransa. Hata hivyo katika muongo wa 1930 Miladia zilianza harakati za kupigania uhuru kwa uongozi wa Habib Bourguiba, na ilipofika mwaka 1957 nchi hiyo ikajipatia uhuru wake huku Bourguiba akiwa rais wa kwanza wa nchi hiyo. Hata hivyo hadi kufikia mwaka 1987 Bourguiba alianza kuiongoza nchi hiyo kwa mabavu na hivyo kupelekea kupinduliwa na Zine El Abidine Ben Ali. Ben Ali ambaye naye pia aliendeleza sera za udikteta na ukandamizaji aling'olewa madarakni kupitia mapinduzi ya wananchi ya mwezi Januari 2011, na kukimbilia Saudi Arabia. Tunisia yenye ukubwa wa kilometa mraba 163,610 iko kaskazini mwa Afrika na inapakana na nchi za Libya, Algeria na bahari ya Mediterania.
&&&
Na siku kama ya leo miaka
35 iliyopita sawa na tarehe 26 Mei mwaka 1981, kulitangazwa rasmi kuundwa
Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi. Baraza hilo linazijumuisha nchi 6 za
kusini mwa Ghuba ya Uajemi ambazo ni Saudi Arabia, Kuwait, Bahrain, Umoja wa
Falme za Kiarabu (Imarati), Qatar na Oman. Malengo ya kuundwa baraza hilo ni
kuimarisha uhusiano wa kiuchumi, kisiasa, kijeshi na kushirikiana nchi
wanachama katika kukabiliana na vitisho vya kigeni.