Apr 24, 2024 03:36 UTC
  • Miili 21 yaopolewa katika ajali ya boti Djibouti

Kwa akali miili 21 imeopolewa kufuatia ajali ya boti katikak pwani ya Djibouti.

Ripoti zinasema kuwa, watu kadhaa wameaga dunia katika maafa mapya ya boti ya wahamiaji kwenye pwani ya Djibouti, shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa liliripoti Jumanne ya jana.

Taarifa zaidi zinasema kuwa, hii ilikuwa ajali ya pili mbaya ya baharini ndani ya wiki mbili kutoka kwenye taifa hilo la Pembe ya Afrika, ambalo liko kwenye ile inayoitwa Njia ya Uhamiaji ya Mashariki kutoka Afrika hadi Mashariki ya Kati.

Meli nyingine iliyokuwa imebeba wahamiaji wengi wa Ethiopia ilizama katika eneo hilo hilo Aprili 8, na kupoteza maisha ya watu kadhaa.

Mkuu wa ujumbe wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji nchini Djibouti, Tanja Pacifico, ameliambia shirika la habari la AFP mjini Nairobi kwamba, miili 21 imepatikana, huku watu 23 wakiwa bado hawajapatikana.

Aidha ameziambia duru za habari kwamba, watu wengine 33 walinusurika kifo kwenye ajali hiyo.